Je, huu ndio mwisho wa Rigathi Gachagua katika siasa za Kenya?

📌 Diğer 📰 BBC Swahili 🕐 4 saat önce
Je, huu ndio mwisho wa Rigathi Gachagua katika siasa za Kenya?

Majaji watatu wa mahakama kuu nchini Kenya Anthony Mrima, Eric Ogola na Freda Mugambi walichukuwa zaidi ya saa kumi Jumatatu ya Juni 8 kutoa uamuazi wao kuhusu hatima ya kisiasa ya aliyekuwa Naibu wa Rais wa nchi hiyo Rigathi Gachagua

Majaji watatu wa mahakama kuu nchini Kenya Anthony Mrima, Eric Ogola na Freda Mugambi walichukuwa zaidi ya saa kumi Jumatatu ya Juni 8 kutoa uamuazi wao kuhusu hatima ya kisiasa ya aliyekuwa Naibu wa Rais wa nchi hiyo Rigathi Gachagua.

Na baada ya kusoma kurasa zaidi ya 300 ya uamuazi huo, watatu hao walionekana kutia msumari moto kwenye kidonda cha Rigathi Gachagua ambaye alikuwa na matumaini makubwa kwamba jina lake lingesafishwa.

Gachagua mwenyewe amesalia kimya na hakufika mahakamani kusikiliza uamuzi wa mahakama na badala yake kuwatuma mawakili wake mahakamani.

Ila alipokuwa kanisani Jumapili Juni 7, kinara huyo wa chama cha DCP alionekana kuashiria kwamba ikiwa dua yake haitapokelewa na malalamishi yake kutupiliwa mbali na mahakama kuu, basi angewaamrisha mawakili wake kujiandaa kuwasilisha kesi mbele ya mahakama ya rufaa.

Kwa mujibu wa sheria za Kenya Gachagua ana siku 14 za kuwasilisha kesi mbele ya mahakama ya rufaa, na siku zingine 30 za kunakili kesi hiyo. Aidha watakaotajwa kwenye kesi hiyo wanapaswa kujulishwa rasmi kisheria katika siku saba za Gachagua kuwasilisha kesi hiyo mahakamani.

Lakini je, baada ya mahakama kuu kutupilia mbali zaidi ya hoja sita kati ya nane alizowasilisha, mahakama ya juu zaidi ina uwezo wa kubatilisha uamuzi wa makahama kuu?

Rais wa chama cha mawakili nchini Kenya, Charles Kanjama anahisi kwamba , ' pande zote zilizohusika kwenye kesi hii zina masuala mengi ya kisheria ambayo yanaweza kujadiliwa mbele ya mahakama ya rufaa.

Baadhi ya masuala ambayo yalizungumziwa na majaji wa mahakama kuu kwa mfano suala la umma kuhusishwa katika mchakato wa kumtimua madarakani afisa wa umma, iwapo suala hilo lilitekelezwa ipasavyo kwa muibu wa katiba na sheria za nchi.

Aidha mahakama iiangazia suala la madai ya Gachagua kwamba umma ulihusishwa kwa maeneo ambayo yaliunga mkono kuondolewa madarakani kwa Gachagua na wala sio maeneo ambayo yalipinga hali hiyo.'

Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.

Kulingana na Naibu Spika wa Bunge la Kitaifa Gadys Boss Sholei ambaye alikuwa anahojiwa na runinga ya Citizen nchini Kenya Jumanne asubuhi, 'Mahakama iliangazia kwa kina hoja zote alizowasilisha Gachagua na kusema kwamba alitendewa haki wakati wa kusikizwa kwa kesi yake bungeni ambapo kulikuwa na uwazi.'

Na huku wengi nchini Kenya hasa katika ngome yake ya siasa za 'Mlima Kenya' wakisubiri kusikiliza kauli yake Gachagua kuhusu hatua atakayoichukuwa, wengi wanajiuliza maswali ikiwa huu ndio mwisho wa siasa zake za upinzani nchini Kenya ambao ndio mwanzo wa mkoko kualika maua.

Mchambuzi wa kis

📌 Kaynak

Bu özet BBC Swahili kaynağından otomatik derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.

Orijinal haberi oku →
📱
News AI World — Mobil uygulama
Bu haberleri 45 dilde, anlık çeviriyle cebinde. Erken erişim için Gmail adresini bırak.
← Tüm haberlere dön