Kombe la Dunia 2026: Mwaka huu ni mashindano kwa ajili ya matajiri pekee?

📌 Diğer 📰 BBC Swahili 🕐 5 saat önce
Kombe la Dunia 2026: Mwaka huu ni mashindano kwa ajili ya matajiri pekee?

Kilio cha mashabiki wa soka kimeshika kasi ulimwenguni kutokana na kupanda kwa bei za tiketi za Kombe la Dunia 2026. Mfumo mpya ulioanzishwa na FIFA umezua mtafaruku mkubwa.

Marekani, Mexico na Canada zinatakuwa wenyeji wa mashindano ya Kombe la Dunia 2026. Timu 48 zitachuana katika viwanja 16 kutafuta mshindi wa mashindano hayo makubwa zaidi ya soka.

Lakini kumezuka malalamiko makubwa kuhusu gharama za kwenda uwanjani na kutazama mashindano haya. Mashabiki hasa nchini Marekani, wanalalamika juu ya bei kubwa ya tiketi.

Ndiposana, wanasheria wakuu wa Serikali wa jimbo la New York na New Jersey nchini Marekani wameanzisha uchunguzi rasmi kuhusu utendaji wa Shirikisho la Soka Ulimwenguni (Fifa).

Mwanasheria mkuu wa New Jersey Jennifer Davenport anasema mchakato huo unatokana na "mkanganyiko, uhaba usio wa kweli viti na bei za juu za tiketi."

Anasema kutakuwa na "uchunguzi wa kina wa mwenendo wa Fifa" huku shirikisho hilo linaloongoza la mpira wa miguu duniani likiitwa kutoa maelezo rasmi.

Davenport alitoa tangazo la pamoja na mwanasheria mkuu wa New York Letitia James na idara ya ulinzi wa watumiaji na wafanyakazi ya Jiji la New York (DCWP).

Kilio cha mashabiki wa soka kimeshika kasi ulimwenguni kutokana na kupanda kwa bei za tiketi za Kombe la Dunia 2026. Mfumo mpya ulioanzishwa na FIFA umezua mtafaruku mkubwa.

Bei za tiketi za mashindano sio tu kwamba ni kubwa kuliko Makombe ya Dunia yaliyopita, pia kwa mara ya kwanza, FIFA imeanzisha bei inayobadilika, na kusababisha bei kuwa juu sana kwa michezo mingi ya Kombe la Dunia.

Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.

Mfano ni kwa mechi ya fainali, iliyopangwa kufanyika New Jersey Julai 19. Awali FIFA iliuza tiketi kwa gharama kubwa ya dola $6,730 — tayari ni kubwa kuliko bei ya dola $1,600 kwa tiketi kwa Kombe la Dunia la FIFA la 2022 huko Qatar.

Kufikia dirisha la mwisho la mauzo kuanzia Aprili, aina hiyo hiyo ya tiketi iligharimu $10,990.

Bei hizo zimesababisha hasira kubwa. Hata Rais Donald Trump wa Marekani, ambaye ana uhusiano wa karibu na Infantino, aliambia New York Post kwamba hawezi kulipa takriban dola 1,000 ili kupata kiti cha kukaaa kwa ajili ya mchezo wa ufunguzi wa Marekani dhidi ya Paraguay mwezi ujao.

Kuzidisha tatizo hilo, FIFA mwezi wa Aprili ilizindua aina mpya kabisa ya tiketi zinazoitwa viti vya mbele. Ni viti vya mstari wa mbele katika uwanja wote, tiketi zimeuzwa kwa bei kubwa kwa viti hivyo.

Kiti cha mstari wa mbele kwenye jukwaa la chini kwa fainali kinagharimu zaidi ya dola $30,000.

Changamoto nyingine kubwa juu ya mauzo ya tiketi za Kombe la Dunia ni kwamba mashabiki hawawezi kuchagua kiti mwanzo mwa mchakato wa kununua tiketi.

Mashabiki wanapewa chaguzi za aina nne za tiketi; baadaye hupewa viti na FIFA

📌 Kaynak

Bu özet BBC Swahili kaynağından otomatik derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.

Orijinal haberi oku →
📱
News AI World — Mobil uygulama
Bu haberleri 45 dilde, anlık çeviriyle cebinde. Erken erişim için Gmail adresini bırak.
← Tüm haberlere dön