Kombe la Dunia 2026: Wachezaji 10 wenye asili ya Afrika wanaopeperusha bendera za Ulaya
Labda tukiite kizazi cha dhahabu. Hawa ndio wachezaji nyota 10 wanaotikisa Ulimwengu wa Soka ambao asili yao ni kutoka Afrika, lakini watacheza kwa niaba ya mataifa mengine
Siku zinazidi kuyoyoma kuelekea michuano ya kihistoria ya Kombe la Dunia 2026, ambalo litafanyika Amerika Kaskazini katika mataifa matatu ya Marekani, Canada na Mexico.
Mataifa 48 yatashindana katika mashindano hayo katika majiji 16. Kwenye viwanja vya mpira 16. Viwanja 11 viko Marekani, vitatu vipo Mexico na viwili vipo Canada.
Mchezo wa soka kwa sasa unashuhudia mabadiliko makubwa ya vizazi. Wakati miungu ya soka kama Lionel Messi na Cristiano Ronaldo wakielekea ukingoni mwa ushindani, uwanja umeachwa wazi kwa ajili ya mashujaa wapya.
Labda tukiite kizazi cha dhahabu. Hawa ndio wachezaji nyota 10 wanaotikisa Ulimwengu wa Soka ambao asili yao ni kutoka Afrika, lakini watacheza kwa niaba ya mataifa mengine mbali na mataifa ya Afrika.
Kylian Mbappé anahesabika kama mmoja wa wachezaji bora duniani kwa sasa. Alizaliwa Desemba 20, 1998, katika kitongoji cha Bondy mjini Paris, Ufaransa, akitokea kwenye familia ya Kiafrika, baba ana asili ya Cameroon na mama ana asili ya Algeria.
Mbappé alipata umaarufu mkubwa akiwa na klabu ya AS Monaco kabla ya kuhamia Paris Saint-Germain (PSG) kwa ada iliyoweka rekodi. Akiwa PSG, alifunga mabao mengi na kuwa mfungaji bora muda wote wa klabu hiyo.
Katika ngazi ya taifa, aliiongoza Ufaransa kutwaa Ubingwa wa Dunia mwaka 2018 akiwa kijana mdogo, na kufunga magoli matatu katika fainali ya Kombe la Dunia ya mwaka 2022.
Baada ya miaka mingi ya uvumi, Mbappé alihamia Real Madrid ya Uhispania, ambako anaendelea kuandika historia yake kwenye klabu kubwa barani Ulaya.
Kinda huyu alizaliwa Julai 13, 2007, huko Esplugues de Llobregat, Uhispania. Mama yake anatokea Guinea ya Ikweta na Baba yake anatokea Morocco. Yamal ni zao la akademia maarufu ya Barcelona, La Masia.
Akiwa na umri wa miaka 15 tu, alicheza mechi yake ya kwanza ya kikosi cha kwanza cha Barcelona, na kuvunja rekodi karibu zote, za kucheza akiwa na umri mdogo katika klabu hiyo na Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga).
Lamine Yamal alishangaza ulimwengu katika michuano ya Euro 2024, ambapo aliongoza timu ya taifa ya Uhispania kutwaa ubingwa huku akitwaa tuzo ya mchezaji mdogo bora wa mashindano.
Uwezo wake wa kuchanja mbuga na chenga za maudhi, na ukomavu wa maamuzi unamfanya kuonekana kuwa mrithi wa Lionel Messi ndani ya Spotify Camp Nou.
Bukayo Saka alizaliwa Septemba 5, 2001, jijini London, Uingereza, kutoka kwa wazazi wenye asili ya Nigeria. Saka ni zao la akademia ya Arsenal (Hale End), na amekuwa ishara ya kufufuka kwa klabu hiyo chini ya kocha Mikel Arteta.
Saka anajulikana kwa nidhamu yake ya hali ya juu, uwezo mkubwa wa kufunga na kutengeneza mabao akitokea
📌 Kaynak
Bu özet BBC Swahili kaynağından otomatik derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.
Orijinal haberi oku →