Sababu tatu zinazozuia meli kupita Hormuz licha ya makubaliano ya Marekani na Iran
"Kufunguliwa kwa mlango huo kunaweza kutokea haraka kwa mtazamo wa kisiasa au kiusalama, lakini kurejea kwa mfumo wa kawaida wa biashara ya meli kutakuwa mchakato wa taratibu," anasema Dimitris Ampatzidis wa Kpler.
Wakati Rais wa Marekani, Donald Trump, alipotangaza makubaliano kati ya Marekani na Iran Jumapili na kueleza kuwa Mlango Bahari wa Hormuz umefunguliwa tena, alihitimisha ujumbe wake kwenye mtandao wake wa Truth Social kwa maneno: "Meli za dunia, washeni injini zenu. Mafuta yaanze kusafirishwa."
Hata hivyo, uchambuzi wa BBC Verify wa takwimu za ufuatiliaji wa meli kutoka MarineTraffic unaonyesha kuwa ni meli saba pekee zinazoonekana kupita katika njia hiyo muhimu ya maji tangu makubaliano hayo yatangazwe. Wakati huohuo, takribani meli 580 zinaonekana kusubiri ndani ya Ghuba ya Uajemi.
Iran ilifunga shuguli zote katika Mlango Bahari wa Hormuz, ambao hupitisha karibu asilimia 20 ya mafuta na gesi ya dunia, kufuatia mashambulizi ya Marekani na Israel ya tarehe 28 Februari.
Wataalamu wanasema bado kuna vikwazo vikubwa vinavyozuia usafiri wa baharini kurejea katika kiwango cha kawaida kilichokuwapo kabla ya mzozo huo. Miongoni mwa changamoto hizo ni masuala ya usalama, mabomu ya baharini na ada za kupita.
Takwimu za MarineTraffic za Jumanne zinaonyesha kuwa zaidi ya meli 250 za kubeba mafuta na zaidi ya meli 330 za mizigo ziko ndani ya Ghuba hiyo.
Takribani asilimia 75 ya meli hizo za mafuta zimesimama bila kusonga. Picha za satelaiti zinaonyesha nyingi zikiwa karibu na vituo vikuu vya usafirishaji wa mafuta nchini Saudi Arabia, Iraq na Falme za Kiarabu.
Idadi halisi ya meli zilizoko katika eneo hilo huenda ikawa kubwa zaidi, kwa kuwa meli nyingi hazitangazi mahali zilipo kupitia mifumo ya ufuatiliaji wa baharini na hivyo hazionekani katika takwimu za MarineTraffic.
Mchambuzi mkuu wa soko la mafuta katika kampuni ya Kpler, Naveen Das, anasema ishara ya kwanza ya kurejea kwa shughuli za kawaida ingekuwa kuanza kwa meli zilizokwama ndani ya Ghuba kuondoka kwa wingi.
"Nahodha atahitaji kuwa jasiri sana kupita katika Mlango Bahari wa Hormuz katika mazingira ya sasa," anasema Martin Kelly wa kampuni ya usimamizi wa migogoro ya EOS Risk Group akiambia BBC Verify.
Tangu Iran ilipoanza kuzuia kwa vitendo matumizi ya mlango huo mwishoni mwa Februari, imekuwa ikifyatua risasi dhidi ya meli zilizojaribu kupita bila ruhusa yake.
Marekani nayo iliweka mzingiro wa kijeshi katika bandari za Iran tarehe 13 Aprili na tangu wakati huo imedai kuzizuia meli tisa ambazo haikuzitambua kama zinazofuata masharti yake, ikiwemo kushambulia vyumba vya injini za baadhi ya meli kwa makombora ya Hellfire.
Ingawa Trump alitangaza kuondolewa mara moja kwa zuio hilo la kijeshi, baadaye alisema utaendelea hadi makubaliano na Iran yatakapotiwa saini rasmi.
Picha za satelaiti za tare
📌 Kaynak
Bu haber XML kaynağından derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.
Orijinal haberi oku →