Kwa nini viongozi wa dini ya Kiislamu wanakamatwa Urusi?
Kuanzia 2023 kumekuwa na mfululizo wa "uvamizi" kwenye maeneo ya ibada ya Waislamu, ambapo wahamiaji walikamatwa na kupelekwa moja kwa moja kwenye ofisi za usajili na uandikishaji wa kijeshi
Vikosi vya usalama vya Urusi hivi karibuni vimewakamata viongozi kadhaa wa dini ya Kiislamu na wanaharakati kadhaa wa kijamii. Vyombo vya habari vya serikali havijaripoti habari hizo, lakini masimulizi mengi kuwahusu yameibuka mtandaoni.
Kwa vyombo vya habari na chaneli za mrengo wa kulia, kukamatwa huku kulikuwa mwanzo wa kampeni iliyosubiriwa kwa muda mrefu ya kuvunja Jukwaa la Kidini la Waislamu wa Shirikisho la Urusi, taasisi inayoungwa mkono na Kremlin inayohusika na kuwawakilisha Waislamu.
Kwa vyombo vya habari vilivyo uhamishoni, matukio haya ni ishara ya kuongezeka kwa chuki dhidi ya Uislamu nchini Urusi, huku wengi wakielekeza kuhusu sheria mpya yenye utata ambayo inapiga marufuku sala za jamaa katika "majengo ya makazi."
BBC Monitoring imechunguza wimbi la kukamatwa, majibu ya viongozi wa dini wa eneo hilo na hatima ya jamii za Kiislamu nchini Urusi.
Ripoti zinaonyesha kwamba viongozi wanane na wawakilishi wa jamii za Kiislamu walikamatwa Mei 2026. Mmoja wao aliachiliwa baadaye.
Miongoni mwa waliokamatwa ni Wissam Bardwill, mufti wa zamani wa eneo la Karelia. Bw. Bardwill alihukumiwa kifungo cha siku 15 jela baada ya kudaiwa "kutotii amri za polisi" katika uwanja wa ndege wa Sheremetyevo Mei 14, shirika la habari la serikali la TASS liliripoti.
Pia, kulingana na ripoti ya chombo cha habari cha ndani cha Furtanga, Mei 12, Huduma ya Usalama ya Shirikisho la Urusi ilimkamata mwanazuoni wa Ingush, Akhmad Tangiyev na naibu wake Wissam Bardwil.
Tovuti maarufu ya habari ya Urusi Lenta.ru iliripoti kwamba Rael Asaynov, mufti wa Jamhuri ya Mordovia, alikamatwa Mei 19 kwa tuhuma za "hongo," akinukuu chanzo cha juu katika Baraza la Mufti la Urusi
Gazeti la biashara la Kommersant lilichapisha orodha ndefu ya wafungwa Mei 23, likinukuu ofisi ya vyombo vya habari ya mahakama na wachunguzi kadhaa ambao hawakutajwa majina.
Kulingana na Kommersant, Mohammad Khani, mkuu wa zamani wa shirika la kidini la Jumuiya ya Waislamu Kaskazini-Magharibi, amekamatwa huko St. Petersburg. Mmoja wa jamaa zake, pamoja na Nidal Awadullah Ahmed, naibu mufti wa eneo la Saratov nchini Urusi, pia walikamatwa.
Tovuti hiyo pia ilichapisha herufi za kwanza na za mwisho za majina ya wafungwa wengine wanne. Chombo cha habari cha uchunguzi "Agentstvo" kiliwatambua kuwa ni wawakilishi wa vituo vya jamii za Waislamu huko Tatarstan, Murmansk na Petrozavodsk.
Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.
Kukamatwa huku kulifanywa kwa sababu mbalimbali kuanzia "hongo" hadi "kutotii," lakini wanablogu na vyombo vya habari viliibua shutuma nzito zaidi.
📌 Kaynak
Bu haber XML kaynağından derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.
Orijinal haberi oku →