Mambo muhimu 14 waliyokubaliana Iran na Marekani
Makubaliano ya Marekani na Iran ya kuongeza muda wa usitishaji mapigano kati ya nchi hizo mbili yamesainiwa na sasa yameanza kutekelezwa, afisa mmoja kutoka ikulu ta White House ameiambia BBC.
Makubaliano ya Marekani na Iran ya kuongeza muda wa usitishaji mapigano kati ya nchi hizo mbili yamesainiwa na sasa yameanza kutekelezwa, afisa mmoja kutoka ikulu ta White House ameiambia BBC.
Rais wa Marekani, Donald Trump, alitia saini makubaliano hayo wakati akihudhuria mkutano wa viongozi wa nchi Tajiri duniani G7 mjini Evian-les-Bains nchini France.
Makubaliano hayo yenye vipengele 14, yanabainisha kuwa Iran haitamiliki silaha za nyuklia. Pia yanaanzisha mfuko wa dola bilioni 300 kwa ajili ya "ujenzi upya na maendeleo ya kiuchumi" ya Iran, ingawa Marekani haitatoa pesa hizo kutoka kwa walipa kodi wake
Makubaliano hayo yanakuja miezi minne baada ya kuzuka kwa mzozo kati ya Marekani na Israel, dhidi ya Iran.
Utawala wa Trump umeelezea makubaliano hayo kuwa yanategemea utendaji ikimaanisha kuwa Iran itanufaika tu ikiwa itatekeleza kikamilifu ahadi zake chini ya mkataba huo.
Ingawa maandishi ya makubaliano hayo yanaacha maswali mengi bila majibu bila kutatua masuala kadhaa muhimu, ila yanaweka msingi wa kuendelea kwa usitishaji mapigano na kufunguliwa tena kwa njia muhimu ya usafirishaji wa mafuta ya Mlango bahari wa Hormuz.
Kifungu cha kwanza cha makubaliano kinaelezea kuwa Marekani, Iran na washirika wao watatangaza kusitishwa kwa operesheni za kijeshi katika maeneo yote ya mzozo, ikiwemo nchini Lebanon.
Kwa upande wa Marekani, Rais Donald Trump amekuwa akionyesha wasiwasi mkubwa kwamba operesheni za kijeshi za Israel dhidi ya kundi la Hezbollah zinaweza kuhatarisha makubaliano yaliyoafikiwa na Iran.
Kwa upande wake, Iran imekuwa ikisisitiza mara kwa mara kuwa Lebanon inapaswa kujumuishwa katika makubaliano ya usitishaji mapigano.
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Kigeni ya Iran alisema Jumatano kuwa kuendelea kwa operesheni za kijeshi za Israel nchini Lebanon kutachukuliwa kuwa ukiukaji wa makubaliano hayo, na kwamba "hatua zinazohitajika zitachukuliwa".
Makubaliano hayo yanaeleza kuwa kuanzia sasa, hakuna upande utakaoanzisha operesheni za kijeshi dhidi ya mwingine wala kutoa vitisho vya kijeshi, na kwamba pande zote zitaheshimu uhuru na mamlaka ya Lebanon.
Hata hivyo, bado haijulikani jinsi Israel itakavyoipokea kipengele hiki cha makubaliano.
Hati hiyo inaelezea kuwa Marekani na Iran zitaheshimu mamlaka ya kila mmoja, mipaka yao, na kuepuka kuingilia mambo ya ndani ya nchi nyingine.
Kwa mujibu wa makubaliano hayo, pande zote mbili zimekubaliana kutoshiriki katika vitendo vinavyoweza kutafsiriwa kama kuingilia siasa za ndani, utawala au masuala ya kitaifa ya upande mwingine.
Hatua hii huenda ikapokelewa kwa mtazamo hasi na makundi ya wapi
📌 Kaynak
Bu haber XML kaynağından derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.
Orijinal haberi oku →