Milio ya risasi yasikika katika uwanja wa ndege wa mji mkuu wa Niger
Niger imekuwa ikipambana na waasi wa Kiislamu kwa muongo mmoja na mwezi Januari watu wanaoshukiwa kuwa wanajihadi walishambulia uwanja huo huo wa ndege.
Meya wa zamani wa Uganda na wakili wa kiongozi wa upinzani anayezuiliwa nchini Kizza Besigye kwa tuhuma za uhaini pia ameshtakiwa kwa kosa linalohusiana na uhaini.
Erias Lukwago alifikishwa mbele ya mahakama ya hakimu mkazi mji katika mkuu Kampala akionekana kuwa dhaifu, vyombo vya habari vya ndani viliripoti, siku chache baada ya kukamatwa nyumbani kwake.
Amekanusha mashtaka dhidi yake na kurudishwa gerezani hadi wiki ijayo kesi yake itakaposikizwa.
Kukamatwa kwake siku ya Jumatatu kulizua shutuma baada ya mkuu wa jeshi la nchi hiyo na mwana wa rais Yoweri Museveni, Jenerali Muhoozi Kainerugaba, kujigamba kwenye mitandao ya kijamii kuhusu tukio hilo.
Mwanasiasa wa upinzani Robert Kyagulanyi maarufu Bobi Wine, ambaye alitoroka nchini Uganda kwa kuhofia maisha yake baada ya kugombea urais wa Januari, alidai kuwa Lukwago alikamatwa kwa amri ya Kainerugaba alipokuwa akijiandaa kuwasilisha wito wa mahakama kwa mkuu wa jeshi.
"Ninatoa wito kwa pamoja kupinga hali hii ya kutokujali sheria," alichapisha kwenye mtandao wa X.
Familia ya Lukwago ilienda mahakamani kudai amri ya kuwalazimisha maafisa wa usalama wanaowatuhumu kumteka kufichua aliko na kumwachilia ikiwa "amekufa au yuko hai".
Familia inasisitiza kuwa Kainerugaba alihusika na kukamatwa kwa Lukwago kwa sababu alijigamba kumdhulumu kwenye mitandao ya kijamii.
Jinsi kiongozi wa upinzani Uganda alivyotoweka nchini Kenya na kuishia katika mahakama ya kijeshi
📌 Kaynak
Bu haber XML kaynağından derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.
Orijinal haberi oku →