Kwa nini aina hizi 11 za saratani zinaangamiza sana vijana?
Saratani za utumbo na matiti ndizo zinazojitokeza zaidi kwa vijana, zikiwa na jumla ya kesi 11,500 kwa mwaka, wakati saratani za kongosho na kibofu cha nyongo ni chache zaidi.
Aina 11 za ugonjwa wa saratani zimeanza kuwa kuwaathiri vijana wengi nchini Uingereza.
Chanzo cha kuongezeka kwa ugonjwa wa saratani bado hakijulikani.
Ila kulingana na utafiti, watu wengi wanazidi kunenepa kupita kiasi, ila hili si hoja pekee.
Wanasayansi kutoka shirika la utafiti wa saratani kutoka taasisi ya Imperial College London, wanasema saratani bado ni adimu miongoni mwa vijana na watu wengi wanaweza kupunguza hatari ya kuambukizwa ugonjwa huo iwapo wataishi maisha yenye afya.
Kwa nini saratani inaongezeka miongoni mwa vijana wa umri wa miaka 20, 30 na 40? ni swali ambalo wanasayansi wamekuwa wakilifanyia utafiti kwa miaka mingi.
Bradley Coombs kutoka eneo la Portsmouth alikuwa na umri wa miaka 23 tu alipofariki kutokana na saratani ya utumbo.
Kulingana na mama yake, Caroline Mausdale, licha ya kuwa mwanawe alikuwa na dalili nyingi za saratani ya utumbo, madaktari walimwona kuwa bado mchanga sana kuweza kuwa na ugonjwa huo.
"Alikuwa kijana mwenye afya nzuri akiwa karibu kusaini mkataba wa soka wa kiwango cha chini kitaalamu,hakukuwa na hatari yoyote"
Hata hivyo, baada ya mwaka wake wa kwanza chuoni, alianza kupungua uzito bila sababu na kupata maumivu ya tumbo. Baadaye, alianza kuharisha na damu ilionekana akienda chooni.
Ilichukua miezi 18 kugundua ugonjwa huo. Alipofanyiwa uchunguzi wa 'colonoscopy', uchunguzi wa video wa utumbo, uvimbe ulikuwa tayari umekua mkubwa kiasi kwamba ulizuia kamera kuingia ndani ya utumbo.
Upasuaji na tiba ya kemotherapi hazikuweza kuzuia ukuaji wa uvimbe huo, na Bradley akafariki dunia.
Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.
Mara nyingi ni vigumu kuua kwanini baadhi ya watu hupata saratani.
Kundi la wanasayansi limechunguza mwenendo wa saratani na mtindo wa Maisha ya watu ili kupata uhusiano kati vitu hivyo na saratani.
Wanasayansi hao waligundua kwamba pamoja na saratani ya utumbo, saratani za tezi ya shingo , multiple myeloma, ini, figo, kibofu cha nyongo, kongosho, endometrium, kinywa, matiti na ovari zinaongezeka.
Saratani za utumbo na matiti ndizo zinazojitokeza zaidi kwa vijana, zikiwa na jumla ya kesi 11,500 kwa mwaka, wakati saratani za kongosho na kibofu cha nyongo ni chache zaidi.
Ni saratani ya utumbo na ovari pekee ambazo zimeonekana kuongezeka hasa kwa vijana, ilhali aina nyingine tisa za saratani pia zimeongezeka kwa watu wazee.
Utafiti uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Saratani na Chuo Kikuu cha Imperial College London pia ulichambua tabia zinazochochea kuongezeka kwa hatari ya kupata saratani.
Utafiti huo ulionyesha kwamba viashiria kama uvut
📌 Kaynak
Bu haber XML kaynağından derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.
Orijinal haberi oku →