Kombe la Dunia 2026: Mbio za taji la mfungaji bora duniani - nani ataibuka kidedea?
Lionel Messi anaongoza kwa mabao matano katika michezo miwili. Kylian Mbappe na Erling Haaland wanashika nafasi ya pili kwenye msimamo wakiwa na mabao manne kila mmoja.
Zinakuwa mbio za kuwania taji la Kiatu cha Dhahabu kwa vizazi.
Lionel Messi anaongoza kwa mabao matano katika michezo miwili. Kylian Mbappe na Erling Haaland wanashika nafasi ya pili kwenye msimamo wakiwa na mabao manne kila mmoja.
Hii ni mara ya pili katika historia ya Kombe la Dunia ambapo wachezaji watatu wamefunga mara nne au zaidi baada ya mechi mbili - na ya kwanza tangu 1954.
Ni wakati mwengine wa ajabu wa kufunga mabao kutoka kwa baadhi ya washambuliaji bora wa kandanda.
Messi alikuwa wa kwanza - akivunja rekodi ya mabao ya Kombe la Dunia kwa kuifungia Argentina mabao mawili dhidi ya Austria.
Mbappe alijibu kwa aina yake kwa mabao mawili katika ushindi wa Ufaransa uliocheleweshwa kwa hali ya hewa dhidi ya Iraq katika mechi yake ya 100 ya kimataifa.
Na ilikuwa zamu ya Haaland baada ya muda mfupi, kufunga mabao mawili Norway ilipoilaza Senegal na kufuzu kwa hatua ya 32 bora. Sio mwanzo mbaya wa maisha ya Kombe la Dunia.
Kitu chochote ambacho mtu anaweza kufanya, wengine wanaweza kufanya vizuri zaidi. Komnbe la Dunia lina hisia hiyo juu yake kwa sasa - na hii ni kabla ya Muingereza Harry Kane kupata kufunga magoli mawili siku ya ufunguzi dhidi ya Ghana Jumanne.
Kuna hisia inayoongezeka tunaona kitu maalum kama rekodi bora zaidi za ulimwengu zinazovunjwa kwenye hatua kubwa zaidi ya mchezo.
Mtaalamu wa soka wa Ufaransa Julien Laurens aliiambia BBC Sport: "Pamoja na nyota wakubwa, wanataka mpira kila wakati.
"Nadhani sehemu yake ni kwamba hawafukuzi tu Kiatu cha Dhahabu, baadhi yao wanafukuza rekodi ya muda wote pia."
Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.
Michuano hii ilianza huku Mjerumani Miroslav Klose akiwa kinara wa wafungaji bora wa muda wote wa Kombe la Dunia akiwa na mabao 16.
Mechi mbili ndani na Messi mwenye umri wa miaka 38 sasa anaongoza kwa mabao 18 katika mechi 28 za Kombe la Dunia, akiwa amefunga mabao yote matano ya Argentina hadi sasa katika toleo hili.
Mfaransa huyo yuko sawa na Klose, amefunga mabao 16 katika mechi nyingi, na atakuwa na mwelekeo wa kuwa mshambuliaji wa kwanza kushinda Viatu vya Dhahabu mara nyingi - kama atakavyofanya Kane - na kuvuka jumla ya Messi.
Laurens alisema: "Tulidhani unaweza kuwa mchuano wa Kylian Mbappe kwa sababu ya rekodi ya ajabu anayowinda, ambayo sasa inamilikiwa na Lionel Messi."
Na ni lini tutazungumzia kuhusu mfungaji mabao wa Manchester City Haaland na rekodi iliopo machoni mwake? Haitakuwa ifikapo mwisho wa mchuano huu - lakini ikiwa ataendelea na kiwango chake cha sasa atakuwa kwenye orodha katika siku zijazo.
Mchezaji huyo mwenye umri wa
📌 Kaynak
Bu haber XML kaynağından derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.
Orijinal haberi oku →