Ni nchi zipi zinazozimiliki ndege muhimu ya kivita aina ya F-35?

📌 Diğer 📰 Kenya 🕐 2 saat önce
Ni nchi zipi zinazozimiliki ndege muhimu ya kivita aina ya F-35?

Nchi zinazoshiriki katika mpango wa F-35 ni Marekani, Uingereza, Italia, Uholanzi, Kanada, Australia, Denmark na Norway.

Rais wa Marekani Donald Trump, akizungumza na waandishi wa habari mjini Ankara kabla ya mkutano wake na Rais Recep Tayyip Erdoğan wa Uturuki, alisema vikwazo dhidi ya Uturuki kupata silaha za ulinzi wa anga zitaondolewa.

Marekani iliweka vikwazo hivyo dhidi ya Uturuki mwezi Disemba mwaka wa 2020 baada ya Uturuki kuamua kununua mfumo wa ulinzi wa anga wa S-400 kutoka Urusi.

Trump alisema watazingatia tena suala la Uturuki kupata ndege za kivita aina ya F-35.

Uturuki ilikuwa miongoni mwa washirika waanzilishi wa mradi wa ndege za F-35.

Hata hivyo, kutokana na sababu hiyo hiyo, Uturuki pia iliondolewa katika mpango wa ndege za kivita aina ya F-35.

Kutokana na hilo, iliibidi Uturuki kuachana na mfumo wa S-400 ili waweze kurejea katika mpango wa ndege za kivita za F-35.

F-35 ni ndege ya kivita ya kisasa yenye matumizi mbalimbali ya kizazi cha tano yenye teknolojia ya hali ya juu, ikiwa na mifumo inayotumia akili mnemba (AI) na uwezo wa kupata taarifa kwa wakati halisi.

Ndege hizi zinaweza kuruka kasi ya takriban kilomita 1,900 kwa saa, lakini hiyo siyo sifa yake kuu.

Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.

F-35 inaweza kugundua na kushambulia malengo kwa uwezo wake yenyewe, huku pia ikikusanya taarifa kupitia mifumo yake na kuzituma kwa ndege nyingine au mifumo mingine ya kivita.

Uwezo huu unachukuliwa kuwa hatua muhimu katika uendeshaji wa operesheni za kisasa za kivita angani. Uwepo wa F-35 katika operesheni husika huongeza kwa kiwango kikubwa uwezo wa ndege za zamani zinazoshiriki katika misheni hiyo.

Ikiwa imeundwa kwa teknolojia ya kuepuka kutambuliwa na ufuatiliaji wa rada, ndege hii inaelezwa kuwa mojawapo ya ndege za kivita zilizo na mifumo ya juu zaidi duniani.

Ndege hii huuzwa takriban dola million 80 za Marekani, n ani miongoni mwa ndege ghali sana za kivita duniani.

Jeshi la Anga la Marekani linasema kuwa toleo la F-35A lina uwezo wa kuhimili nguvu ya 9g .

Hii ina maana kwamba rubani anaweza kustahimili nguvu ya mivutano(gravity) inayofikia mara tisa ya nguvu ya kawaida ya uvutano wa dunia wakati wa kufanya mizunguko au miondoko ya kasi angani.

Kwa sasa, F-35 ndiyo mpango mkubwa na wenye gharama kubwa zaidi wa utengenezaji wa silaha za kivita duniani.

Mpango huo unatarajiwa kuendelea kwa takriban miaka 30 hadi 40.

Ripoti ya majaribio ya Pentagon iliyowekwa wazi kwa umma mnamo mwezi Novemba 2024 inaelezea kuwepo kwa wasiwasi kuhusu ucheleweshaji wa kutengeneza ndege hizo, usahihi wa silaha zinazoundwa, na uwezo wa mfumo wa ulinzi dhidi ya mashambulizi ya mtandaoni.

Kwa mujibu wa mpango wa F-35,

📌 Kaynak

Bu haber XML kaynağından derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.

Orijinal haberi oku →
📱
News AI World — Mobil uygulama
Bu haberleri 45 dilde, anlık çeviriyle cebinde. Erken erişim için Gmail adresini bırak.
← Tüm haberlere dön