Nyuma ya pazia ya urembo unaokuwa wa kukuza makalio

📌 Diğer 📰 Kenya 🕐 7 saat önce
Nyuma ya pazia ya urembo unaokuwa wa kukuza makalio

Sindano za vipodozi hapo awali zilihusishwa na watu matajiri, wa umri wa makamo wanaotafuta matibabu ya kupunguza kuzeeka, lakini urembo huo umeenea katika muongo mmoja uliopita.

Alice Webb alipokwenda kuongeza makalio ya Ki-Brazil (BBL) bila upasuaji - utaratibu unaohusisha kudungwa sindano ya kujaza jeli kwenye matako - katika kliniki moja mwezi Septemba 2024, alitarajia kumaliza kwa wakati na arudi nyumbani.

Mama huyo wa watoto watano alifariki chini ya saa 24 baada ya kudungwa sindano, na kuwa mtu wa kwanza nchini Uingereza kujulikana kufariki kufuatia zoezi hilo. Uchunguzi utafanyika katika msimu wa vuli ili kubaini chanzo cha kifo chake.

Hadithi yake imekuwa kitovu cha mjadala unaokua kuhusu tasnia ya urembo inayokua nchini Uingereza, ambapo sindano za urembo sasa zinapatikana kila mahali, kuanzia saluni za urembo, ofisi na vyumba vya hoteli.

Katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, nimechunguza tasnia hii, nikifanya uchunguzi wa siri ili kujua kinachoendelea.

Nilikutana na wataalamu ambao walikuwa tayari kuingiza mamia ya mililita za jeli mwilini mwangu kutoka katika vyumba vya matibabu vya muda katika majengo ya ofisi. Nilipewa dawa bila ushauri unaofaa wa daktari na kuuziwa sindano za kupunguza uzito zisizo na lebo kwenye mitandao ya kijamii.

Nimezungumza na wanawake kadhaa ambao wameniambia kuhusu maumivu makali waliyoyapata yaliyosababishwa na sindano za vipodozi ambazo hutangazwa kuwa hazina maumivu na hazina hatari, na maambukizi yaliyotokana na hayo yaliyowapeleka hospitalini.

Huduma ya uidhinishaji wa vipodozi Save Face inasema imeshuhudia visa vingi vya madhara makubwa vinavyohusishwa na matibabu ya urembo - ikiwa ni pamoja na mgonjwa mmoja ambaye aliachwa bila uwezo wa kufunga macho yake baada ya upasuaji wa kope uliokwenda vibaya, na mwingine ambaye aliyetoboka utumbo wakati wa kufyonzwa mafuta.

"Ni jambo la kutisha sana, ni kama aina fulani ya filamu ya kutisha, lakini hizi ni taratibu zinazofanywa katika mitaa yetu," anasema mkurugenzi wa Save Face Ashton Collins.

Uingereza ni mojawapo ya masoko ya sindano za vipodozi yenye udhibiti. Tofauti na nchi nyingi za Ulaya, mtu yeyote anaweza kufunzwa kuingiza jeli kwenye ngozi na kutoa matibabu kwa umma.

Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.

Juni 2024 Joanne (ambaye anataka tutumie jina lake la kwanza tu) alikwenda kuchomwa sindano ya kuongeza makalio katika kliniki moja huko Essex kwa sababu aliona ni hatari kwenda Uturuki kwa ajili ya upasuaji - hii ilikuwa kabla ya Alice kufariki.

"Nilitaka tu makalio makubwa," anasema Joanne, mama wa watoto wawili kutoka South Wales. Muda mfupi baada ya matibabu, ambapo alidungwa sindano ya lita 1 (painti 1.8) ya jeli, aliishia hospitalini akiwa na maambukizi kwenye damu. Miaka

📌 Kaynak

Bu haber XML kaynağından derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.

Orijinal haberi oku →
📱
News AI World — Mobil uygulama
Bu haberleri 45 dilde, anlık çeviriyle cebinde. Erken erişim için Gmail adresini bırak.
← Tüm haberlere dön