Trump atishia Iran usitishaji mapigano "umefutiliwa mbali"; Iran yaonya kuwa "watajibu bila uwoga"
Trump alipokuwa akiuita uongozi wa Iran kuwa "wakihuni" na "unaougua", Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran alisema: "Hatulipizi matusi kwa matusi, bali kwa vitendo."
Trump alipokuwa akiuita uongozi wa Iran kuwa "wakihuni" na "unaougua", Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran alisema: "Hatulipizi matusi kwa matusi, bali kwa vitendo."
Trump ameulizwa na vyombo vya habari kuhusu kauli yake ya mwezi uliopita kwamba watu wa Iran walikuwa wema na wenye nia njema kushirikiana nao — ikilinganishwa nay eye leo kuwaita viongozi wa Iran "wahuni".
Alijibu kwa kusema kuwa "amewafahamu", akiongeza kuwa viongozi wa nchi hiyo hawawafanyii wananchi wao jambo jema "kwa kuzingatia matendo yao katika wiki moja au mbili zilizopita."
Trump kisha alisema haamini kuwa mzozo mkubwa utaanza tena, akiongeza kuwa: "Chochote kitakachotokea kitaisha haraka sana."
Rais huyo alirudia kauli zake za awali kwamba Marekani "inaweza" kuishambulia Iran usiku huu.
Aliongeza kuwa mtu yeyote atakayekaribia nyenzo za nyuklia za Iran zilizohifadhiwa chini ya ardhi "atalipuliwa", na kwamba Marekani hatimaye "itazichukua."
Trump ameulizwa katika mkutano na wanahabari ikiwa anaonekana kama vita vinaweza kuanza tena.
"Nadhani hali itamalizika haraka sana. Washambulie meli kadhaa, na sisi tuwashambulia kwa nguvu zaidi."
Ameongeza kuwa awali aliulizwa kama alikuwa anapanga kuishambulia Iran tena, na akasema: "Nilisema tunaweza kufanya hivyo, ndiyo, tunaweza."
"Lakini wanaposhambulia, nasi tunashambulia," alisema. "Tunatumia lugha yao na tunazungumza lugha yao."
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ametoa taarifa ikishutumu Marekani kwa kukiuka Hati ya Maelewano (MoU) — makubaliano kati ya Iran na Marekani ya kushirikiana kumaliza mzozo huo.
Wizara hiyo imetaja kile ilichokiita "mashambulizi haramu ya mara kwa mara dhidi ya Iran, pamoja na uamuzi wa Waziri ya Fedha wa Marekani jana usiku wa kufuta leseni ya uuzaji wa mafuta ya Iran" kuwa ni miongoni mwa ukiukaji huo.
Imeonya kuwa Marekani inawajibika kwa "athari mbaya" zinazosababishwa na kuongezeka kwa mvutano huu.
Pakistan, mpatanishi wa Marekani na Iran ataka pande zote kujizuia
Pakistan imeeleza wasiwasi wake mkubwa kuhusu kuongezeka kwa mvutano katika eneo la Mashariki ya Kati.
Nchi hiyo ilikuwa miongoni mwa wapatanishi wakuu waliofanikisha kutiwa saini kwa Hati ya Maelewano (MoU) kati ya Marekani na Iran mwezi uliopita, baada ya kuwa mwenyeji wa mazungumzo ya ngazi ya juu yaliyofanyika mnamo mwezi Aprili.
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje alisema, "mgogoro mpya sio kwa maslahi ya upande wowote", na akatoa wito kwa "pande zote kujizuia" na kutekeleza ahadi zao katika Hati ya Maelewano (MoU).
Taarifa hiyo inasema: "Hakuna njia mbadala ya kuendelea kushirikiana, zaidi ya kufanya mazungumzo, na kutumia diplomas
📌 Kaynak
Bu haber XML kaynağından derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.
Orijinal haberi oku →