Kwa nini Uturuki iliwazawadia viongozi wa NATO bastola zenye risasi sita?

📌 Diğer 📰 Kenya 🕐 7 saat önce
Kwa nini Uturuki iliwazawadia viongozi wa NATO bastola zenye risasi sita?

Zawadi hiyo ya bastola iliwekwa ndani ya kisanduku cha mbao chenye mpangilio wa rangi nyeusi. Kisanduku hicho kilikuwa na bendera ya Uturuki, nembo ya NATO na kibao kilichoandikwa kwa Kituruki na Kiingereza: "Gumusay, bastola ya kwanza ya aina ya revolver kutengenezwa nchini mwetu."

Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, aliwashangaza viongozi wa NATO kwa kuwapa kila mmoja bastola iliyokuwa na risasi sita kama zawadi mwishoni mwa mkutano wa muungano huo uliofanyika Ankara.

Kila bastola ilikuwa imechongwa jina la kiongozi aliyepokea zawadi hiyo pamoja na jina la nchi yake. Hata hivyo, baadhi ya viongozi hawakuweza kuondoka nazo kutokana na sheria za nchi zao kuhusu silaha za moto.

Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer, alilazimika kuiacha bastola hiyo mikononi mwa maafisa wa Uingereza nchini Uturuki kwa sababu sheria za Uingereza haziruhusu kuingiza silaha za moto nchini humo.

Kansela wa Ujerumani, Friedrich Merz, na Waziri Mkuu wa Uholanzi, Dick Schoof, pia hawakuzichukua zawadi zao.

Waziri Mkuu wa Canada, Mark Carney, alipoulizwa alifikiria nini alipoiona zawadi hiyo, alisema kwa utani kuwa hakuwahi hata kuifungua na kusisitiza kuwa hapendi kuwa karibu na silaha.

"Nataka kuwahakikishia Wakanada kwamba silaha iliwekwa mbali nami."

Aliongeza kuwa zawadi hiyo haikuwa kile alichotarajia. "Nadhani, ikilinganishwa na sharubati ya maple niliyokuwa nimetoa kama zawadi… iwe ilikuwa bastola ya kalibu .357 au kitu kama hicho, haikulingana na haikuwa zawadi inayofaa."

Sharubati ya maple, inayotengenezwa kutokana na utomvu wa mti wa maple, ni kitamu cha asili kinachotumika kama kiungo cha kuongeza utamu wa vyakula na vinywaji.

Aliongeza kuwa, "Jambo lingine lililonijia akilini ni kwamba hiki ni kitu ambacho kingefaa kuhifadhiwa katika makumbusho ya vita, au makumbusho ya Jeshi la Canada, au mahali pengine pa aina hiyo, ambako kingekuwa cha kuvutia na pia chenye umuhimu katika kuelezea historia na nafasi ya NATO kwa ujumla."

Baadaye Carney alisema bastola hiyo imekabidhiwa kwa Polisi wa Farasi wa Kifalme wa Canada na imeondolewa uwezo wa kutumika, kwa kuwa haikidhi masharti ya kisheria ya kumilikiwa nchini humo.

Waziri Mkuu wa Canada aliongeza, "Kwa kweli, haikuwa zawadi niliyotarajia."

Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.

Waziri Mkuu wa Ubelgiji alifahamu kuhusu bastola hiyo baada ya ndege yake kutua Brussels na akaikabidhi mara moja kwa polisi wa uwanja wa ndege.

Pia Ofisi za mawaziri wakuu wa Uholanzi na Uswidi zilisema bastola walizopewa zimehifadhiwa katika balozi za nchi zao mjini Ankara. Bastola ya Uholanzi ilitarajiwa kuondolewa uwezo wa kutumika, huku ile ya Uswidi ikisubiri kukamilishwa kwa taratibu za kuingizwa nchini humo.

Kwa upande wa Waziri Mkuu wa Italia, Giorgia Meloni, bastola yake tayari imehifadhiwa katika Palazzo Chigi, makao makuu ya serikali ya Italia, pamoja na zawadi

📌 Kaynak

Bu haber XML kaynağından derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.

Orijinal haberi oku →
📱
News AI World — Mobil uygulama
Bu haberleri 45 dilde, anlık çeviriyle cebinde. Erken erişim için Gmail adresini bırak.
← Tüm haberlere dön