Zelensky apendekeza mazungumzo ya ana kwa ana na Putin ili kumaliza vita vya Ukraine

📌 Diğer 📰 BBC Swahili 🕐 1 saat önce
Zelensky apendekeza mazungumzo ya ana kwa ana na Putin ili kumaliza vita vya Ukraine

Kupitia barua ya wazi aliyomwandikia Putin, Zelensky alisema kuwa ni muhimu viongozi hao wawili kukutana moja kwa moja ili kujadili njia za kurejesha amani kati ya Urusi na Ukraine.

Mwanahabari wa Marekani ambaye alikuwa akiishi na kufanya kazi nchini China kwa zaidi ya muongo mmoja amekiri hatia katika mahakama ya Marekani kwa kufanya kazi kama wakala haramu wa Jamhuri ya Watu wa China (PRC).

Thomas Weir Pauken II, 50, “alikiri kuwa sehemu ya njama ya kupata taarifa nyeti kutoka serikali ya Marekani” kwa niaba ya China, alisema Naibu Mwanasheria Mkuu wa Marekani anayehusika na usalama wa taifa, John A. Eisenberg.

Nyaraka za mahakama zinaonesha kuwa Pauken alikuwa akiishi China tangu mwaka 2010 na alikuwa amefanya kazi na mashirika kadhaa ya vyombo vya habari huko, ikiwa ni pamoja na China Central Television na Xinhua News.

Kwa mujibu wa nyaraka hizo, Pauken alifanya kazi “kwa maelekezo na udhibiti wa watu aliowajua kuwa wanahudumu kwa niaba ya PRC” kuanzia mwaka 2019 hadi Februari mwaka huu.

Miongoni mwa watu aliowasiliana nao ni mtu anayejulikana kama “Cathy”, ambaye Wizara ya sheria ya Marekani (DOJ) ilisema alimpa “maelekezo, ikiwa ni pamoja na kukutana na watu wanaoweza kuwa vyanzo vya taarifa za kijasusi”.

Pauken na “Cathy” walitambulishwa na mtu aliyekuwa mwandishi wa hotuba wa Rais wa China Xi Jinping wakati wa “vita vya biashara kati ya Trump na China” mwaka 2017, kulingana na nyaraka za mahakama.

DOJ ilisema mwanahabari huyo wa Marekani alipokea takribani dola 100,000 kutoka kwa “Cathy” kwa kazi hiyo.

Pauken pia aliagizwa kusafiri mara kadhaa kati ya mwaka 2019 na 2025 kukutana na watu nchini Marekani ambao wangeweza kumpa taarifa za kuzipeleka kwa PRC.

Mwanahabari huyo wa Marekani “alikusanya taarifa za kiintelijensia kuhusu watu aliolenga Marekani na kuzipeleka kwa wasimamizi wake wa ujasusi wa China,” alisema Mkurugenzi Msaidizi Roman Rozhavsky wa Kitengo cha Ujasusi na Usalama wa Ndani cha FBI.

Rozhavsky aliongeza kuwa kesi hiyo ni mfano wa “hatua kubwa ambazo Chama cha Kikomunisti cha China kiko tayari kuchukua ili kudhoofisha taasisi zetu za kidemokrasia na kupunguza uhuru wetu wa kisiasa”.

Pauken alifanya kazi na watu wengine wawili nchini China, wanaotambuliwa kama “William” na “Richard”, ambao walimwambia mwanahabari huyo kwamba ripoti alizowaandikia zilikuwa zikipelekwa Japan.

Pia Pauken alitoa kwa kundi la watu kutoka Wuhan taarifa kuhusu Wizara ya Sheria ya Marekani (DoJ) na taarifa kuhusu teknolojia. Pia waliomba Pauken awasaidie kupata mtaalamu wa kuwasaidia katika kufanya ujasusi wa kimtandao.

Baada ya kusikilizwa kwa kesi hiyo Alexandria, Virginia, wakili wa Pauken, Charles Burnham, alitoa taarifa kwa Politico iliyosema mteja wake anakubali kuwajibika na alikuwa akijaribu “kukuza uhusiano wa ama

📌 Kaynak

Bu özet BBC Swahili kaynağından otomatik derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.

Orijinal haberi oku →
← Tüm haberlere dön