Kijiji ambacho watu husafiri kilomita 45 kuchaji simu zao
Maafisa husika wanasema kutounganisha umeme katika Kijiji hicho kunatokana na hali mbaya ya barabara.
Kwa Kulsooma, msichana mwenye umri wa miaka 19 kutoka Kijiji cha Vandiji iliyopo kwenye milima ya Himalaya, wilaya ya Kupwara Kashmir, suala la utandawazi na Maisha ya kisasa, ni mambo anayoyasikia, kwani maisha yake ni sawa na ya watu wa kale.
Vizazi vitano vya Kijiji cha Vandiji hawajahi kuwa na nguvu za umeme, na kizazi cha sasa kinakuwa pia kwa kutumia mwanga wa stovu au jiko la mafuta na mishumaa.
Kijiji hicho kimekuwa kikisubiria kupata umeme kwa miongo kadhaa ila hawajafanikiwa hadi kufikia sasa.
Sio tu njia pekee ndiyo mbovu kufika katika Kijiji hicho, ila Maisha ya wakaazi hao pia ni magumu.
Baada ya kufanya kazi mchana kutwa, jioni ikifika, changamoto mpya zinawakabili.
"Wanawake hapa wana wasiwasi sana kwa sababu mchana wanakumbwa na moshi kutoka kwenye majiko wanayopikia, na usiku moshi kutoka kwenye taa au mishumaa wanayotumia kusomea huwasababishia maumivu," anasema Kulsooma.
Anaelezea kuwa anapoondoka kijijini hapo, mara moja yeye huhisi kama si sehemu ya ustaarabu wa kisasa wa binadamu.
"Tunapokwenda sokoni Kupwara, tunajihisi duni tunapoona watu wakiwa na simu zao za kisasa. Tunapotembelea nyumba za ndugu,tunaona vifaa vya umeme vya kisasa. Inatufanya tuhisi kama, sisi ni watu wa kale wanaoishi katika nyakati za kisasa."
Kutokana na ukosefu wa barabara na umeme, wakaazi wa eneo hilo huishi kwa kukwea milima.
Wilaya ya Kupwara ipo kilomita 75 kaskazini mwa Srinagar. Kijiji cha Vandiji kipo kilomita 45 kutoka mji wa Kupwara, na inaweza kufikia kwa kutumia usafiri wa gari.
Ila watu hukwea millima hadi kufikia makazi yao. Na katika safari hii tulikutana na Bashir Ahmed Mir, ambaye alikuwa amebeba vyombo vya nyumbani begani.
Anatuelezea kuwa "huwa tunabeba vyombo vya nyumbani na bidhaa nyingine kutoka Kupwara na usiku tunakutana barabarani tukiwa na tochi, hakuna barabara, hakuna umeme, nikama serikali haijui Kijiji cha Vandiji kiko wapi"
Wakaazi wa eneo hilo huteremeka na kukwea milima kueleka mji wa Kupwara kuchaji simu zao ili waweze kuzungumza na jamaa zao, iwapo kuna dharura.
Ila huduma ya mtandao wa mawasiliano kwa njia ya simu ni duni sana.
Ukosefu wa umeme umewaathiri pakubwa kiafya wakazi wa Kijiji hicho.
Abdul Rashid Malik, amekuwa akipokea matibabu kwa miaka miwili sasa. Anaugua ugonjwa wa moyo kutokana na kifua chake kuathirika.
"tunachoma kuni nyingi kila siku, haiharibu tu nyumba yetu bali pia afya yetu. Nilianza na kukohoa, kisha daktari akaniambia nina maambukizi ya kifua na baadaye ikabainika moshi unaathiri moyo wangu"
Abdul aliongezea kuwa "iwapo kungekuwa na umeme hakuna mmoja wetu angekuwa mgonjwa. Kuanzi
📌 Kaynak
Bu özet BBC Swahili kaynağından otomatik derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.
Orijinal haberi oku →