Je, Elon Musk kuwa trilionea wa kwanza duniani?

🚀 Uzay 📰 BBC Swahili 🕐 4 saat önce
Je, Elon Musk kuwa trilionea wa kwanza duniani?

Iwapo hisa za kamuni hiyo zitauzwa zaidi ya dola 135, itakuwa mojawapo ya makampuni tajiri duniani. Hilo likitokea na Musk ambaye anamiliki 80% ya Space X anaweza kuwa trilionea.

Kampuni ya Elon Musk, Space X, imetangaza bei ya hisa ya kampuni hiyo kabla ya kufungua hisa hizo kwa umma.

Ikiwa wataweza kufikia bei lengwa, kampuni hiyo itakuwa ya kwanza kuuza hisa kubwa kwa umma kuwahi kutokea katika historia.

Kulingana na taarifa ya kampuni hiyo iliyotolewa tarehe 3 mwezi Juni, hisa za space x zitauzwa dola 135, na itailetea kampuni hiyo kipato cha dola trillioni 1.75.

Si kawaida kutangaza kipato cha kampuni kabla ya hisa kuuzwa.

Taarifa ya kampuni hiyo si hakikisho kuwa hisa hizo zitauzwa kwa makadirio hayo, bali inategemea na uamuzi wa wanunuzi. Bei hiyo inaweza kupanda au kushuka.

Space X ambayo hujenga roketi na vifaa vingine vya angani na pia inamiliki XAi na Starlink, imechukua hatua isiyo ya kawaida ya kutangaza bei ya hisa kwa umma kabla ya kuanza kuuza kwa umma wiki moja baadaye.

Kwa kawaida kampuni nyingi hutangaza bei yao siku moja kabla ya kuanza kuuza hisa.

Hisa za Space X zinatarajiwa kuanza kuuzwa katika soko la hisa la NewYork la Nasdaq kuanzia tarehe 12 mwezi Juni, na kuifanya kuwa kampuni ya kwanza kwenye historia kutoa makadirio ya bei ya hisa kabla ya kuanza kuuza.

Kampuni hiyo inalenga kupata mtaji wa dola billioni 75 kupitia uuzaji wake wa kwanza wa hisa kwa umma, hii ikiwa rekodi mpya ya juu.

Rekodi ya awali inashikiliwa na kampuni ya mafuta ya Saudi Aramco ambayo ilipata mtaji wa dola billioni 25.6 mwaka wa 2019.

Iwapo hisa za kamuni hiyo zitauzwa zaidi ya dola 135, space X itakuwa mojawapo ya makampuni tajiri duniani. Hilo likitokea na Musk ambaye anamiliki 80% ya Space X anaweza kuwa trilionea.

Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.

Kwa mujibu wa takwimu za kampuni ya utafiti wa masoko ya Dealogic, karibu nusu ya kampuni zote zilizotoa hisa zao kwa umma,katika kipindi cha miaka 30 iliyopita zimepoteza thamani tangu zilipoanza kuuza kwenye soko la hisa.

Samuel Kerr, mtendaji wa kampuni ya Mergermarket alisema kuhusu SpaceX kuwa "Bila shaka thamani yake imepandishwa kwa kiwango cha juu sana."

Thamani ambayo SpaceX imejiwekea ikilinganishwa na mauzo yake ni kubwa zaidi kuliko ile ya kampuni nyingine yoyote katika kundi la kampuni kubwa za teknolojia linalojulikana kama "Mag 7", linalojumuisha, Amazon, Apple, Meta, Nvidia, Microsoft na Tesla.

Kerr aliongeza kuwa, "Hata hivyo, SpaceX inathaminiwa kwa kuzingatia mapato na faida zinazotarajiwa siku zijazo badala ya hali yake ya sasa, hivyo baadhi ya wawekezaji wanaweza kupuuza hali hiyo."

Mwaka uliopita, kampuni ya Space Exploration Technologies (SpaceX) ilipata mapato ya dola bilioni 18.6 lakini ikarekodi has

#space

📌 Kaynak

Bu özet BBC Swahili kaynağından otomatik derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.

Orijinal haberi oku →
← Tüm haberlere dön