Iwapo Iran na Marekani wataafikia makubaliano, Israel itakuwa na chaguo gani?
Ikiwa mazungumzo yatagonga mwamba, Israel huenda italazimika kutegemea kampeni ya muda mrefu inayohusisha operesheni za kijeshi na za siri ili kuzuia Iran kupata silaha za nyuklia.
Juhudi za kufikia makubaliano kati ya Marekani na Iran bado zinaendelea, huku Israel ikijadili uwezekano wa makubaliano kuafikiwa na athari zake.
Swali kuu si iwapo makubaliano yataafikiwa, ni nini Israel itafanya iwapo Tehran na Washington wataafikia makubaliano?
Vyombo vya habari na wataalam wa usalama wameacha kuhoji kuhusu makubaliano hayo, na sasa wanataka Israel ijiandae kukabiliana na matokeo ya Marekani kukubaliana na Iran, haswa kuhusu uhuru wa jeshi la Israel na mpango wa nyuklia wa Iran.
Israel inahofia kuwa makubaliano yatakayoafikiwa ni sawa na ile ya JCPOA, ambayo itadhibiti mpango wa nyuklia, lakini itatoa uhuru wa kuendelea na mpango wa makombora na ndege zisizo na rubani.
Gazeti moja la Israel lilichapisha taarifa na kusema kuwa makubaliano yatakayoafikiwa hayatakuwa yameafikia malengo hitajika ya kulemaza nguvu za kijeshi za Tehran, mfumo wake na washirika wake wa karibu.
Kulingana na gazeti hilo, Israel haina haja na ushindi kamili dhidi ya Iran, bali wanataka hakikisho kutoka Washington kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran na Hezbolllah.
Ila Israel bado hawajakubaliana jinsi ya kukabiliana na changamoto hii na inasemekana kuwa inamsumbua akili Waziri mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu.
Danny Citrinovich mtafiti wa masuala ya ulinzi ambaye awamehi kuhudumu katika idara ya ujasusi ya Israel,anasema kuwa,iwapo makubaliano hayataafikiwa haraka, utawala wa Trump utaanza kuchoka, na hali huenda ikawa kama ya awali ambapo hakuna vikwazo kuhusu nyuklia ya Iran, au hatua yoyote itakayochukuliwa na Marekani, na baadaye ushawishi wa Tehran utakuwa katika eneo hilo.
Watu wengi Israel wanaona kuwa mkataba wowote utakaoafikiwa utakuwa mbaya, kwani vita hivyo bado havijaafikia malengo ya Tel Aviv na Washington
Tofauti hii ya maoni inaonyesha mgawanyiko uliopo katika wataalam wa usalama na wachambuzi wa Israel. Makubaliano yanaweza yasiwe ya kuifaa Israel, lakini kushindwa kabisa kwa mazungumzo hayo kunaweza pia kusababisha hali hatari zaidi, kulingana na baadhi ya wachambuzi
Katika mazingira kama hayo, Israel inakabiliwa na njia mbalimbali za kuchukua hatua.
Mojawapo ya hatua ambazo Israel inaweza kuchukua ni kujaribu kuvuruga maandishi ya mwisho ya mkataba wa makubaliano.
Mshauri wa zamani wa usalama wa taifa wa Israel, Yaakov Amidror, alinukuliwa akisema kwamba matakwa makuu ya Israel katika makubaliano yoyote na Iran yanapaswa kuwa, kusitishwa kwa urutubishaji wa urani na kuwekwa vikwazo kwenye mpango wa makombora wa Iran.
Kulingana na matakwa haya, Israel inaweza kufanya makubaliano kati ya Marekani na Iran kuwa magumu zaidi na yenye gh
📌 Kaynak
Bu özet BBC Swahili kaynağından otomatik derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.
Orijinal haberi oku →