Hezbollah yapinga makubaliano mapya ya usitishaji vita kati ya Israel na Lebanon
Marekani ilitangaza makubaliano ya kusitisha mapigano Jumatano usiku kufuatia duru mpya ya mazungumzo.
Marekani ilitangaza makubaliano ya kusitisha mapigano Jumatano usiku kufuatia duru mpya ya mazungumzo.
Kundi la wapiganaji la Hezbollah nchini Lebanon limepinga vikali masharti ya usitishaji vita kati ya Israel na Lebanon unaoungwa mkono na Marekani.
Katika taarifa yenye maneno makali, kiongozi wa kundi linaloungwa mkono na Iran Naim Qassem alisema mazungumzo hayo "hayana msingi" na "ya kufedhehesha" kwa Lebanon, na kuongeza kuwa sehemu kubwa ya Welebanon "kinadharia" wanapinga mazungumzo haya.
Kauli yake inajiri saa kadhaa baada ya Israel na Lebanon kutangaza upya usitishaji wa mapigano kwa makubaliana kwamba "Hezbollah watapigwa marufuku.
Katika taarifa ya pamoja iliyotolewa Jumatano na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, nchi hizo tatu zilisema makubaliano hayo "yanategemea kusitishwa kabisa" kwa mashambulizi ya Hezbollah.
Lakini akijibu siku ya Alhamisi, kiongozi wa Hezbollah - ambayo haikuwa sehemu ya mazungumzo - alisema "usitishaji mapigano unaotarajiwa", uliotafsiriwa na Israel kama Hezbollah kuweka chini silaha na kuwaondoa wapiganaji kutoka kusini mwa Lebanon ni sawa na kuslimu amri na hatua hiyo itatimiza malengo ya Israel.
Kiongozi huyo Hezbollah pia alionya kwamba maadamu vijiji vya Lebanon vinashambuliwa kwa mabomu, eneo la kaskazini mwa Israel halitakuwa salama.
Saa kadhaa kabla ya hapo, Rais wa Lebanon Joseph Aoun alitaja usitishaji mapigano uliosimamiwa na Marekani kuwa fursa ya mwisho ya amani ya kudumu nchini Lebanon.
Wakati huo huo Israel imesisitiza kuwa usitishaji vita hautazuia mashambulizi yake ya ardhini dhidi ya Hezbullah.
Kwa nini ngome hii yenye miaka 900 ni muhimu katika vita vya Israel-Hezbollah?
Kwa nini ndege ndogo zisizo na rubani za Hezbollah zimekuwa tatizo kwa Israel?
Rais wa Marekani Donald Trump amewasuta wabunge waliopiga kura ya kudhibiti mamlaka yake, akiwataja kuwa watu "wasio wazalendo".
Siku ya Jumatano, Bunge la Wawakilishi la Marekani lilipitisha azimio la kumzuia Trump kuchukua hatua zaidi za kijeshi nchini Iran.
Katika chapisho katika mtandao wake wa kijamii wa Truth Social, rais huyo aliandika: "Jana Bunge lilipiga kura isiyo na maana ili kupunguza mamlaka yanya, nikiwa katika harakati za mwisho za kumaliza Vita na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Ni nani angefanya jambo lisilo la kizalendo kama hilo?"
Pia imeelezea uamuzi huo kama jaribio lisilo la kikatiba la kudhibiti mamlaka ya rais.
Kura hiyo ambayo iiliungwa mkono na wabunge 215 dhidi ya 208, ilikuwa ya kupitisha azimio la kudhibiti mamlaka ya kivita, ambalo lingemtaka Trump kuondoa majeshi ya Marekani au kutafuta idhini ya bunge kushughul
📌 Kaynak
Bu özet BBC Swahili kaynağından otomatik derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.
Orijinal haberi oku →