Moto wafufua mjadala wa CCTV mashuleni, usalama kwanza au faragha?
"CCTV ni shahidi wa kimya, haiwezi kuzuia tukio kutokea, lakini inaweza kusaidia kubaini ukweli baada ya tukio kutokea'', anasema mtaalamu wa faragha ya data Philip Kisaka.
Katika siku za hivi karibuni, kisa cha kamera fiche ya CCTV ilivyonasa wanafunzi saba wakishukiwa kupanga njama ya kuchoma bweni iliyoua wanafunzi 16 katika shule ya upili ya wasichana ya Utumishi Academy nchini Kenya kimeibua mjadala mkali.
Baadhi wameeleza kuwa video hii ilileta ufunuo wa kilichosababisha moto huo huku wengine wakihisi kwamba kamera fiche za CCTV kuwekwa kwa bweni ni kuingilia faragha ya wanafunzi wa kike.
Hata hivyo, Mtaalamu wa masuala ya faragha ya data Philip Kisaka anasema kuna maeneo ambayo mtu anatarajiwa kuwa na faragha kamili, kama vile vyumba vya kulala, bafu, msalani na vyumba vya kubadilishia nguo. Katika maeneo hayo, matumizi ya CCTV yanaweza kukiuka haki ya faragha inayolindwa na Katiba ya Kenya pamoja na Sheria ya Ulinzi wa Data.
"Msingi mkuu ni kwamba lazima kuwe na sababu halali ya kutumia kamera. Huwezi kufunga CCTV mahali ambapo watu wanatarajia kufanya shughuli zao binafsi bila kufuatiliwa," anasema Philip.
Akiiambia BBC Swahili kuwa iwapo wazazi wa shule ya Utumishi waliridhia na wanafunzi walijua kuna kamera fiche haiwezi kuchukuliwa faragha yao iliingiliwa.
''Pia vigezo vingine vitatumika kujua haki ya faragha ya wanafunzi ilikiukwa ni kubainishwa kuwa matumizi ya CCTV katika bweni hilo yalikuwa yanalenga nini'', anaendelea kueleza.
Hii ndiyo kanuni inayojulikana kama purpose limitation, yaani taarifa zinapaswa kukusanywa kwa sababu maalum na kutotumika nje ya kusudi hilo. Hili limeainishwa kutoka kwa sheria ya ulinzi wa data 2019.
"CCTV ni shahidi wa kimya, haiwezi kuzuia tukio kutokea, lakini inaweza kusaidia kubaini ukweli baada ya tukio kutokea'', anasema mtaalamu wa faragha ya data Philip Kisaka.
Kwa mujibu wa katiba ya Kenya kifungu cha 31 kinasema kuwa kila raia ana haki ya kuwa na faragha hasa maeneo binafsi na mawasiliano binafsi kuwekwa wazi.
Baada ya tukio hilo waziri wa usalama wa ndani Kenya Kipchumba murkomen aliwashauri wasimamizi wa shule za bweni kufunga CCTV na ziwe na wafanyakazi wa kufuatilia kinachoendelea kama njia ya kiusalama.
''Ni muhimu kwa wasimamizi wa shule kuchukua hatua na kufunga kamera fiche ambazo zinafuatiliwa ili kuepuka majanga shuleni'' alisema Murkomen akirejelea mkasa wa moto katika shule ya Utumishi.
Hata hivyo kamishna wa data za faragha ameonya kuwa kuwekwa kwa CCTV kwa mabweni inaibua kuingilia faragha ya wanafunzi.
Ikiwa kamera imewekwa katika eneo la biashara au sehemu ya umma kwa sababu za usalama, si lazima kila mtu apewe ruhusa binafsi kabla ya kurekodiwa. Hata hivyo, sheria inataka watu wafahamishwe kuwa eneo hilo lina CCTV.
Ndiyo maana katika majengo
📌 Kaynak
Bu özet BBC Swahili kaynağından otomatik derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.
Orijinal haberi oku →