Kwanini Kim Jong-un huwa hamzungumzii mama yake?

🏥 Sağlık 📰 BBC Swahili 🕐 1 gün önce
Kwanini Kim Jong-un huwa hamzungumzii mama yake?

Ko alifariki kabla ya Kim Jong-il, ila kifo chake katika hospitali moja mjini Paris hakikutajwa na vyombo vya habari vya Korea kaskazini.

Katika mambo mengi fiche kuhusu kiongozi wa Korea kaskazini, Kim Jong Un, suala la mama yake mzazi limesalia fiche.

Tangu kuchukua madaraka miaka 15 iliyopita, Kim hajawahi kumtaja mamake waziwazi.

Tofauti na viongozi wawili wa awali wa Korea Kaskazini Kang pan sook mamake Kim il-Sung na Kim Jong-Sook mamake Kim Jong-Il, walikuwa wanaitwa "mama wa Korea".

Ila mamake Kim jong Un, Ko Yong-hui, hajaonekana hadharani wala hakuna majengo yaliyopewa jina lake kama njia ya heshima.

Kufichwa kwa Ko Yong-hui, kunaonekana kutokana na alikotoka na pia kuwa hawara, mambo ambayo wachambuzi wanasema huenda ikaathiri utawala wa kiongozi huyo.

Kulingana na waandika wasifu, Ko alizaliwa Osaka Japan mwaka wa 1952, kutoka kwa wazazi waliokuwa wakaazi wa kisiwa cha Jeju ambayo kwa sasa inamilikiwa na Korea kusini.

Kwasababu familia yake iliishi Japan, Ko alikuwa "zainishi mkorea" jina walilopewa wakorea walioishi eneo hilo wakati wa ukoloni wa Japan kati ya mwaka 1910-1945.

Wakorea wengi waliwaonea wivu wale waliokuwa wakirejea kutoka Japan kipindi hicho, kwani walirejea na pesa nyingi pamoja na vifaa vya nyumba.

Ila pia waliitwa "jaebo" jina la kudunisha kwa kudai watu waliotoka Japan walikuwa na mawazo mabaya ya kigeni.

Nchini Korea kaskazini, kuna matabaka ya watu na Wakorea Zainichi wanatajwa kuwa watu wasiokuwa na tabaka halisi na wanaweza kusababisha uhasama.

Watu kutoka kundi hili, hufuatiliwa kwa karibu na serikali na mara nyingi wananyimwa nafasi katika vyuo vikuu au ajira.

Korea kaskazini ni jamii yenye ngazi tofauti ambayo si rahisi kubadilisha tabaka lako.

Dkt Jung Young-tae kutoka chuo kikuu cha Dongyang, anasema jamii hiyo pia imeundwa kwa mfumo wa "mtu kuwa na hatia sababu ya undungu" ambapo raia wanaweza kuadhibiwa kwa matendo yaliyofanywa na wanafamilia wao.

Ko alipokuwa na umri wa miaka 10, familia yake ilirejea Korea Kaskazini.

Familia yake ilikuwa miongoni mwa wakorea 93,000 waliohama kutoka Japan na kurejea katika taifa hilo la kikomunisti, kupitia mpango wa kuwapa maisha bora wanaorejea Korea Kaskazini ikiwemo kazi na elimu ya bure.

Ila Ko alibahatika kuepuka maisha ya umaskini na kuteseka ambayo ilikuwa inawasubiria wakorea zainichi wengi, baada ya kupendwa na kiongozi wa wakati huo Kim Jong-il.

Ingawa hakutambulishwa rasmi kama mke wa kiongozi huyo, inasemekana rais huyo tayari alikuwa amemuoa Kim Yong-Suk, binti ya mwanajeshi mmoja mkuu, ndoa amabyo ilikuwa imepangwa na babake.

Ko alikuwa miongoni mwa kundi la densi, na alimvutia kiongozi huyo kutokana na urembo wake na ujuzi wake wa densi.Hii ni kulingana na kitabu alichochapisha m

#hospital

📌 Kaynak

Bu özet BBC Swahili kaynağından otomatik derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.

Orijinal haberi oku →
← Tüm haberlere dön