WARIDI WA BBC: Akiwa na miaka 12 alitafutiwa mume wa miaka 50, leo ameokoa mabinti 300

📰 Gündem 📰 BBC Swahili 🕐 2 gün önce
WARIDI WA BBC: Akiwa na miaka 12 alitafutiwa mume wa miaka 50, leo ameokoa mabinti 300

Sikuelewa mengi kuhusu ndoa, lakini nilielewa jambo moja maisha yangu yalikuwa yanabadilishwa bila ridhaa yangu.

Usiku ule bado naukumbuka vizuri. Nilikuwa na miaka 12 tu, nimemaliza shule ya msingi kijijini kwetu Ngorongoro. Wakati watoto wengine walikuwa wanaota ndoto za kuendelea na masomo, mimi nilikuwa nimeandaliwa kuolewa na mwanaume aliyekuwa na umri wa miaka 50.

Sikuelewa mengi kuhusu ndoa, lakini nilielewa jambo moja maisha yangu yalikuwa yanabadilishwa bila ridhaa yangu.

Kaka yangu Fredy ndiye aliyekuwa mwanga wangu. Alibahatika kupata elimu na kuona dunia tofauti na ilivyo kijijini kwetu. Aliposikia wazee wakipanga ndoa yangu kwa siri, alinifuata na kuniambia:

"Theresia, lazima uondoke hapa kama unataka kuendelea kusoma."

Theresia anasema usiku uliofuata alitoroka nyumbani kwa siri.

'Nilikuwa mtoto mdogo mwenye hofu kubwa moyoni, sijui ninakoenda wala nini kitanikuta mbele. Nilitembea na kusafiri kutoka Ngorongoro hadi Arusha mjini, safari iliyoonekana ndefu lakini nilikuwa nina matumaini ya kupata msaada huko'.

Nilifika Arusha majira ya saa kumi na moja jioni nikiwa nimechoka, mwenye njaa na hofu.

Alipokelewa na sista wa kanisa Katoliki aliyemsitiri na kumpeleka katika kituo cha kuwahudumia watoto wa kike wa kimasai waliokuwa wamekimbia changamoto, alieleza Theresia

Nilipewa nafasi ya kuendelea na masomo. Kadri nilivyokuwa nakua, ndivyo nilivyozidi kuelewa kuwa wasichana wengi wa kimasai walikuwa wanapitia maumivu yale yale tohara, ndoa za utotoni, kunyimwa elimu na kukosa nafasi ya kuamua maisha yao.

Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.

Baada ya kuhitimu elimu ya sekondari, mwaka 2014 Theresia alijiunga na Same School of Nursing na kusomea uuguzi kwa muda wa miaka mitatu.

Mafunzo hayo yalimpatia msingi mkubwa wa kuwahudumia wagonjwa na kuelewa changamoto mbalimbali za afya zinazowakabili wanawake na watoto katika jamii.

Anaeleza kwamba kadri alivyoendelea kufanya kazi hospitalini, alizidi kuguswa na maumivu wanayopitia wanawake wakati wa kujifungua na wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji.

'Hapo ndipo nilipoamua kuongeza utaalamu zaidi katika eneo la dawa za usingizi'.

Mwaka 2019 alijiunga na chuo cha KCMC kusomea utaalamu wa dawa za usingizi na ganzi (Anaesthesia).

Mafunzo hayo yalimfanya kuwa mtaalamu wa dawa za usingizi na ganzi, taaluma inayohusika na kuhakikisha wagonjwa wanapata huduma salama na kupunguza maumivu wakati wa upasuaji au kujifungua.

Theresia ambaye sasa ni mwanamke anayetazamwa kama mfano kwa jamii ya kimasai anasema tangu akiwa mdogo, alivutiwa sana na wahudumu wa afya.

'Nakumbuka kila nilipokuwa nikienda hospitali na kuona wauguzi au madaktari wakifanya kazi zao kwa utulivu na huru

#war

📌 Kaynak

Bu özet BBC Swahili kaynağından otomatik derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.

Orijinal haberi oku →
← Tüm haberlere dön