Rosana Kathure: "Ningejua anayenioa atanikata jicho, nisingeolewa"

📌 Diğer 📰 BBC Swahili 🕐 4 gün önce
Rosana Kathure: "Ningejua anayenioa atanikata jicho, nisingeolewa"

Rosana anasema mume wake alikuwa akimuambia maneno makali kila walipokwazana lakini yeye aliyachukulia kirahisi.

Mwanamke anapotoka kwao na kuamua kuolewa huwa anajua amepata mwenza wake akiwa na matumaini ya kuishi naye kwa shida na raha hadi kifo kitakapowatenganisha.

Lakini inakuwaje pale unapogundua kuwa aliyekutoa kwenu amebadilika na kuwa mtu tofauti kabisa na badala ya kuishi pamoja kwa upendo ikageuka sio tu karaha lakini kiasi cha hata kunusurika kifo kwa tundu ya sindano.

Katika Waridi wa BBC, Asha Juma alipata fursa ya kuzungumza na Rosana Kathure kutoka eneo la Meru nchini Kenya aliyepitia ukatili katika ndoa yake.

Rosana Kathure anakumbuka wakati alipokutana na baba watoto wake mtarajiwa wakati huo upendo ndio ulikuwa umetawala.

Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.

Baada ya kipindi kifupi cha kuchumbiana, waliamua kwenda kwa wazazi ili kurasimisha ndoa yao.

Rosana anasema maisha kabla ya mtafaruku kati yake na mume wake, walipenda kama chanda na pete.

"Kabla ya huu mkasa kutokea, tulikuwa tunakunywa na glasi moja ya chai. Kaupendo kalikuwa kazuri sana," kwa tabasamu la aina yake Rosana anasema.

"Kuna wakati alikuwa anakuja akiwa mlevi, nilimchukua nikamtoa viatu na kumuosha miguu. Kisha nikampandisha kitandani akalala. Nilikuwa nampenda," Rosana anaongeza.

Lakini kulingana na simulizi ya Rosana, mume wake alibadilika baada ya miaka kadhaa.

"Mtu hakuonyeshi mambo mabaya wakati uko kwenu. Lakini ubaya huanza pole pole hadi inapofikia wakati hali inakuwa mbaya zaidi," anasema Rosana.

"Mtoto wa kwanza na wa pili, mume wangu alikuwa sawa. Mtoto wa tatu akiwa na miezi minne, mume wangu alianza kubadilika. Alianza kuvuta bangi na kunywa chang'aa. Alikuwa akinipiga bila sababu, vita kila wakati ndani ya nyumba hadi anamwaga chakula jikoni. Na mimi pia nikaanza kelele," Rosana anakumbuka.

Rosana anakiri kuwa baada ya kuona tabia za mume wake zimebadilika, hata yeye alianza kuwa mama mwenye kelele na kila wakati alikuwa akimwambia mume wake kwamba atarudi kwao. Ila majibu ya mume wake yalikuwa makali ingawa kwake aliyachukulia kirahisi.

"Alikuwa akiniambia kuliko nitoke hapa na kurudi kwetu, ni heri yeye aniuwe na ajiue," Rosana anakumbuka majibu ya mume wake kila walipokwazana.

Rosana alikuwa amezoea kusikia maneno hayo masikioni mwake kila wakati.

Mambo yalibadilika kabisa alipofingua mtoto wake wa mwisho na alipotimiza miezi miwili, kile ambacho hakikutarajiwa kikatokea.

Rosana anasema hakujua kama siku hiyo maisha yake yangechukua mwelekeo mpya.

Hali ilikuwa kama kawaida na ratiba ya Rosana siku hiyo ilikuwa kumpeleka kliniki. Aliamka na kujitayarisha na kumuacha mume wake na watoto wengine watatu.

Si

📌 Kaynak

Bu özet BBC Swahili kaynağından otomatik derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.

Orijinal haberi oku →
← Tüm haberlere dön