Afrika kuanza kutumia Su-34M, ndege mpya za kivita za Urusi
Su-34M ni ndege ya kivita ya Urusi ambayo ni ya mashambulizi ya masafa marefu , iliyotengenezwa kwa ajili ya mashambulizi ya ardhini, baharini na pia kujilinda angani.
Afrika imeingia katika hatua mpya ya ushindani wa kijeshi baada ya kuibuka kwa taarifa za kuwasili kwa ndege za kivita za Urusi aina ya Su-34M katika kikosi cha anga cha Algeria.
Hatua hiyo imezua mjadala mpana kuhusu iwapo bara hilo linaingia kwenye awamu mpya ya mbio za silaha, huku mataifa kadhaa yakiendelea kuwekeza katika teknolojia za kisasa za kivita.
Wachambuzi wa masuala ya ulinzi wanasema ujio wa ndege hizo hauwezi kuangaliwa kwa mtazamo wa nchi moja pekee, bali kama sehemu ya mabadiliko ya kimkakati yanayoendelea Afrika Kaskazini na bara zima. Hii ni kutokana na ukweli kwamba mataifa mengine pia yanaimarisha vikosi vyao vya anga na mifumo ya makombora, hali inayoongeza ushindani wa kijeshi katika eneo hilo.
Kwa sasa, Su-34M inaonekana kuwa moja ya alama mpya za ushawishi wa kijeshi wa Urusi barani Afrika, hasa katika nchi zinazotegemea zaidi silaha zake za anga.
Swali kubwa linaloulizwa ni kama ujio wa ndege hizi utabadilisha kwa kiasi kikubwa uwiano wa nguvu za kijeshi au ni sehemu nyingine ya mzunguko wa kawaida wa biashara ya kisasa ya silaha duniani?
Su-34M ni ndege ya kivita ya Urusi ambayo ni ya mashambulizi ya masafa marefu , iliyotengenezwa kwa ajili ya mashambulizi ya ardhini, baharini na pia kujilinda angani.
Ndege hii hutengenezwa na kampuni ya Sukhoi chini ya shirika la serikali la UAC (United Aircraft Corporation) nchini Urusi.
Ingawa msingi wake ni Urusi, Su-34M imekuwa sehemu ya mpango mkubwa wa usafirishaji wa silaha za Urusi kwa washirika wake wa kijeshi. Hata hivyo, bado matumizi yake makubwa yako ndani ya jeshi la anga la Urusi, ambapo imekuwa ikitumika katika operesheni mbalimbali za kijeshi katika miaka ya hivi karibuni.
Kuhusu Afrika, Algeria inaonekana kuwa miongoni mwa nchi chache za kwanza barani humo kupokea au kuhusishwa moja kwa moja na ndege hizi za kisasa. Hii inaifanya kuwa tukio la kipekee, kwani nchi nyingi za Afrika bado zinategemea zaidi ndege za vizazi vya zamani au mifumo ya magharibi na Urusi ya awali kama MiG na Su-30.
Kwa ujumla, upatikanaji wa Su-34M unaashiria hatua ya juu ya ushirikiano wa kijeshi kati ya Urusi na baadhi ya mataifa ya Afrika, lakini bado si mwelekeo wa bara zima kwa sasa.
Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.
Su-34M imeundwa kwa ajili ya operesheni za mashambulizi ya mbali dhidi ya maeneo ya kimkakati, ikiwa na uwezo wa kubeba mzigo mkubwa wa silaha ikiwemo mabomu ya kawaida na pamoja na makombora ya masafa marefu. Inaweza kufanya safari ndefu bila kujazwa mafuta mara kwa mara, hali inayoiwezesha kufikia malengo ya mbali.
Ndege hii pi
📌 Kaynak
Bu özet BBC Swahili kaynağından otomatik derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.
Orijinal haberi oku →