Kauli tata za wanasiasa wanaohama vyama Tanzania

📌 Diğer 📰 BBC Swahili 🕐 29.05.2026
Kauli tata za wanasiasa wanaohama vyama Tanzania

Ingawa kisheria kuhama chama ni haki ya kikatiba ya kila mwanasiasa, mjadala mkubwa hubaki kwenye maneno waliokuwa wakiyasema wakati wakiwa kwenye vyama wanavyovihama, maneno ambayo mara nyingi huonekana kugongana na hatua zao za baadaye.

Mabadiliko ya uhamaji wa kisiasa nchini Tanzania yameendelea kuwa chanzo cha mijadala mikali ya kitaifa, hasa pale wanasiasa wanapohama kutoka chama kimoja kwenda kingine na baadaye kurejea tena walikotoka. Matukio ya hivi karibuni ya Joseph Selasini, Peter Msigwa na Patrick Assenga yameibua upya mjadala kuhusu kauli zao walizowahi kuzitoa wakiwa ndani ya vyama walivyovihama na baadaye kurejea.

Msigwa, ambaye alikuwa CHADEMA na baadaye kuhamia CCM kabla ya kurejea tena CHADEMA wiki hii, Selasini aliyewahi kuondoka CHADEMA kwenda NCCR-Mageuzi na sasa kutangaza kurejea CHADEMA, pamoja na Assenga aliyepitia CHAUMA kabla ya kurudi CHADEMA, wote wamechangia kuibua maswali kuhusu uthabiti wa misimamo ya kisiasa na kauli zao za zamani.

Ingawa kisheria kuhama chama ni haki ya kikatiba ya kila mwanasiasa, mjadala mkubwa hubaki kwenye maneno waliokuwa wakiyasema wakati wakiwa kwenye vyama wanavyovihama, maneno ambayo mara nyingi huonekana kugongana na hatua zao za baadaye.

Wapo pia wanasiasa wengine waliopitia njia hiyo hiyo, akiwemo Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa, ambaye alihama CCM kwenda CHADEMA na baadaye kurejea CCM, Wilbroad Slaa, Katibu Mkuu wa zamani wa CHADEMA aliyeenda CCM kabla ya kuwatosa tena, hali inayoongeza uzito wa mjadala huu wa kisiasa wa "kauli dhidi ya matendo."

Kwa ujumla, uhamaji wa vyama umekuwa sehemu ya siasa za Tanzania, lakini kinachobaki akilini mwa wananchi ni kauli tata za viongozi hao, kauli ambazo mara nyingi hubadilika kulingana na mazingira ya kisiasa wanayokutana nayo.

Peter Msigwa, mbunge wa zamani wa Iringa Mjini na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ni miongoni mwa wanasiasa waliowahi kutoa kauli zinazoleta utata. Wakati akiwa CHADEMA aliyekaa kwa muda mrefu alipoulizwa na chombo kimoja cha habari kama atahamia CCM alisema:

"Siwezi kuuza utu wangu kwa vipande 30 vya fedha au cheo… CCM siendi, bora nisiwe Mbunge."

Kauli hiyo aliitoa Disemba 30, 2023 akiwa kiongozi wa CHADEMA. Hata hivyo, baadaye mwaka 2024 alihamia CCM, kabla ya kurejea CHADEMA wiki hii.

Akiwa CHADEMA, Msigwa pia alikuwa akiikosoa sana CCM kuhusu demokrasia na katiba, pamoja na masuala kama utekaji na usalama kwa ujumla, lakini baadaye akiwa CCM alibadilisha msimamo na kusema wananchi wako salama chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan.

Akitangaza kurejea CHADEMA alihusisha pia matukio ya usalama akisema:

"Matukio hayo yaliniumiza na kunifanya nishindwe kuendelea kuishi katika huzuni kubwa na ukimya."

Septemba 7, 2024, alipokuwa akifanya mahojiano na Kipindi cha Medani za Siasa cha Star TV, alisema “nuru im

📌 Kaynak

Bu özet BBC Swahili kaynağından otomatik derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.

Orijinal haberi oku →
← Tüm haberlere dön