WARIDI WA BBC: 'Nilitokwa na haja ndogo bila kukoma kwa miaka minne'

📰 Gündem 📰 BBC Swahili 🕐 27.05.2026
WARIDI WA BBC: 'Nilitokwa na haja ndogo bila kukoma kwa miaka minne'

Shirika la afya ya uzazi la Umoja wa Mataifa - UNFPA na Wakfu wa Fistula wanakadiria kuwa visa vipya vya fistula 1,000 hadi 3,000 hutokea nchini Kenya kila mwaka.

Kwa miaka mingi, aliishi kwa kujificha na ukimya usio kifani, alihisi aibu kutokana na kile alichokuwa anakipitia.

Nasuri yaani fistula tatizo ambalo huathiri maelfu ya wanawake kila wakati hasa barani Afrika.

Shirika la afya ya uzazi la Umoja wa Mataifa - UNFPA na Wakfu wa Fistula wanakadiria kuwa visa vipya vya fistula 1,000 hadi 3,000 hutokea nchini Kenya kila mwaka.

Ugonjwa huu mara nyingi hutokana na kutoweza kupata matibabu ya dharura wakati mama mjamzito anapokuwa kwenye chumba cha kujifungua.

Katika Waridi wa BBC hii leo, Asha Juma amezungumza na Annifah Adhiambo ambaye amekabiliana na ugonjwa huu kwa miaka 4.

Annifah anasema siku ya kwenda kujifungua kila kitu kilikuwa sawa lakini ghafla akasikia madaktari wakinong'onezana neno ambalo lilimuacha na wasiwasi.

"Nilikuwa na uchungu kama kawaida, lakini nilivyoenda kujifungua nikasikia madaktari wakisema, mtoto amechoka sana inafaa niende kufanyiwa upasuaji na bahati mbaya mtoto alikuwa amechoka kiasi kwamba alitoka akiwa amekufa," Annifah anasema.

Kile ambacho Annifah hakukijua ni kuwa mtoto huyo alimuacha na ugonjwa wa fistula ingawa wakati huo hakujua ni nini. Lakini alichokuwa anakiona machoni pake kilikuwa kinamtia hofu.

"Nilikuwa ninaona damu ikitoka, haitoki peke yake, inatoka na maji fulani hivi, kitu kilichokuwa tofauti, hadi ninashangaa haya maji yanatoka wapi na ni maji ya nini na hayakuwa yameanza kutoa harufu ambayo ingenifanya nihisi kuwa ni mkojo," Annifah anasema.

Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.

Na baada ya miezi miwili, Annifa ndio alijua kuwa kile anachokiona sio maji bali ni mkojo.

"Nilikuwa nimeenda kliniki kuangaliwa jinsi ninavyoendelea kwa sababu ya upasuaji, na hapo ndipo nilipomsimulia daktari kile ninachopitia. Moja kwa moja akaniarifu kuwa ni ugonjwa unaojulikana kama fistula lakini unatibika," Annifa anasema.

Annifah anazungumzia alichoanza kukumbana nacho baada ya kutoka hospitalini.

"Ninakumbuka tu kuona mkojo ikinitoka. Hayo maji yalikuwa yanatoka tu, siwezi kuhisi kwenda haja ndogo," Annifah anaongeza.

"Mikojo yangu ilikuwa inamalizikia mahali nimekaa. Nikiketi itatoka, nikisimama itatoka, nikitembea itatoka. Sikuwa ninahisi kwamba ndiyo hiyo inatoka bali nitahisi tu nimeloa," anakumbuka Annifah.

"Kwa miaka minne sikunywa chai wala maji. Ningekula chakula chochote lakini maji haikuwa rahisi ninywe kwa sababu nilifikiri kadiri ninavyokunywa maji ndivyo mikojo inavyotoka. Nilikuwa nikijiambia hivyo lakini huo haukuwa ukweli. Mikojo ilikuwa inatoka tu hata kama sijakunywa maji wala chai," anasema Annifah.

"Mwan

#war

📌 Kaynak

Bu özet BBC Swahili kaynağından otomatik derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.

Orijinal haberi oku →
← Tüm haberlere dön