Ni nani anayelinda meli eneo la Ghuba na Bahari ya Shamu?
Je, ni miungano gani maarufu zaidi ya kijeshi kwa sasa inayolinda usafiri wa baharini katika eneo la Mashariki ya Kati?
Baada ya Iran kuendelea kuudhibiti Mlango Bahari wa Homuz, kama hatua ya kulipiza kisasi mashambulizi ya Marekani na Israel dhidi yake mnamo Februari 28, Uingereza na Ufaransa zimekuwa zikiongoza juhudi za usalama baharini kulinda biashara za kimataifa katika ukanda huo muhimu ambapo asilimia 20 ya mafuta duniani husafirishwa.
Hivi majuzi Uingereza na Ufaransa, pamoja na nchi nyingine 24, zilitangaza kuunga mkono kuanzishwa kwa ujumbe "huru wa kujihami" wa jeshi la kimataifa ili kuondoa mkwamo katika Mlango-Bahari wa Hormuz, kwa mujibu wa sheria za kimataifa, wakati masharti yanayofaa yatakapotimizwa.
Nchi hizo 26 zilisema katika taarifa ya pamoja iliyotolewa na Wizara ya Ulinzi ya Uingereza baada ya London na Paris kufanya mkutano wa mawaziri wa ulinzi na wawakilishi kutoka nchi 38 mnamo Mei 12 na kutangaza uungaji mkono wao kwa ujumbe huu, ambao unalenga kuzihakikishia usalama kampuni za biashara za meli na kutekeleza shughuli za kuondoa vilipuzi vya chini ya maji.
Je, ni miungano gani maarufu zaidi ya kijeshi kwa sasa inayolinda usafiri wa baharini katika eneo la Mashariki ya Kati?
Combined Task Force 153, ambayo kwa sasa inaongozwa na Misri, ilianzishwa Aprili 17, 2022. Ni mojawapo ya vikosi vitano vya Jeshi la Wanamaji la Combined Marine Corps (muungano wa kimataifa wa kutoa ulinzi baharini), kufuatia matukio katika Bahari Shamu, hasa kurushwa kwa kombora kutoka eneo linalodhibitiwa na Houthis nchini Yemen.
Kutoa ulinzi katika Bahari ya Shumu, Bab al-Mandab na Ghumba ya Aden, na kukabiliana na shughuli haramu, magendo na uharamia.
Combined Task Force 153, inayoongozwa na Australia, ilipeleka meli nne zisizo na rubani kati ya Februari na Aprili 2026, zikishika doria katika eneo la shughuli zenye ukubwa wa kilomita za mraba 219,000, zinazofunika karibu nusu ya Bahari ya Shamu, kufuatilia shughuli zozote zisizo halali.
Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.
Kikosi cha wanamaji cha EU "ASPEDS" ni misheni ya baharini iliyotumwa katika Bahari ya Shamu. Ilianzishwa mnamo Februari 2024 kama operesheni ya kujihami ili kukabiliana na mashambulizi ya mara kwa mara wapiganaji wa Kihouthi dhidi ya meli za kimataifa tangu Oktoba 2023, na mamlaka ya awali ambayo yanafanywa upya kila mwaka. Mamlaka yake yameongezwa hadi tarehe 28 Februari 2027.
Majadiliano yanaendelea ndani ya Umoja wa Ulaya kupanua majukumu ya Operesheni Aspidis kujumuisha Mlango-Bahari wa Hormuz.
Kulinda meli na kuhakikisha uhuru wa urambazaji katika Bahari ya Shamu, Ghuba ya Aden, Bahari ya Arabia, Bahari ya Oman, Ghuba, na Kaskazini Magharibi mwa
📌 Kaynak
Bu özet BBC Swahili kaynağından otomatik derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.
Orijinal haberi oku →