Ebola ni nini na kwa nini kuzuia mlipuko huu ni vigumu sana?
Mlipuko wa Ebola katika Democratic Republic of the Congo unahusisha aina adimu ya virusi na unatokea katika eneo lililoathiriwa na migogoro.
Mlipuko wa ugonjwa wa Ebola nchini DRC umetangazwa kuwa dharura ya afya ya umma ya kimataifa na WHO.
Kukabiliana na mlipuko huu ni jambo gumu kwa sababu Inahusisha aina adimu ya virusi ambayo haina chanjo, na visa vya ugonjwa huo vimegunduliwa katika eneo lililoathiriwa na migogoro.
Ebola ni ugonjwa adimu lakini hatari unaosababishwa na virusi.
Virusi vya Ebola kwa kawaida huambukiza wanyama, hasa popo wa matunda, lakini milipuko kwa binadamu wakati mwingine huanza pale watu wanapokula au kushika wanyama walioambukizwa.
Huchukua siku mbili hadi 21 kwa dalili kujitokeza. Dalili huanza ghafla na kufanana na mafua, kama vile homa, maumivu ya kichwa, na uchovu.
Kadiri ugonjwa unavyoendelea, mgonjwa hutapika na kuharisha, na hali inaweza kusababisha viungo vya mwili kushindwa kufanya kazi.
Baadhi ya wagonjwa, lakini si wote, hutokwa damu ndani ya mwili na nje ya mwili.
Virusi hivyo huenea kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine kupitia kugusana na majimaji ya mwili yaliyoambukizwa kama damu au matapishi.
Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.
Mlipuko huu unasababishwa na aina ya Ebola inayojulikana kama Bundibugyo, ambayo haikuwa imeonekana kwa zaidi ya muongo mmoja.
Aina ya Bundibugyo imesababisha milipuko miwili tu hapo awali, ambapo iliua takribani theluthi moja ya watu walioambukizwa.
Vipimo vya awali vya damu vya Ebola vilionesha matokeo hasi kwa sababu vipimo hivyo hutambua zaidi aina za kawaida za virusi hivyo.
Hakuna chanjo iliyoidhinishwa kwa Ebola ya Bundibugyo, lakini chanjo za majaribio zinaendelea kutengenezwa.
Inawezekana kwamba chanjo ya aina nyingine ya Ebola inayoitwa Zaire inaweza kutoa kinga fulani.
Pia hakuna dawa zilizotengenezwa mahsusi kutibu Bundibugyo, jambo ambalo linafanya matibabu kuwa magumu zaidi.
Changamoto nyingine ni kwamba mlipuko huu unatokea katika eneo lenye migogoro, ambapo karibu watu laki mbili na hamsini wamekimbia makazi yao, na watu wengi wanavuka mipaka isiyodhibitiwa kuelekea nchi jirani.
Hata hivyo, tangazo la WHO kwamba huu ni dharura ya afya ya umma ya kimataifa halimaanishi kuwa dunia iko katika hatua za mwanzo za janga kama la COVID-19. Hatari ya Ebola kuenea nje ya Afrika Mashariki ni ndogo sana.
Kisa cha kwanza kilichojulikana kilikuwa cha muuguzi aliyepata dalili tarehe 24 Aprili, jambo linaloonesha kwamba virusi vilikuwa vinaenea bila kugunduliwa kwa wiki kadhaa.
Hii ina maana kwamba ukubwa halisi wa mlipuko huo haujulikani, na kazi ya kuwatafuta wagonjwa walioambukizwa pamoja na watu ambao huenda waliwaambukiza wengine imekuwa ngumu zaidi.
Muuguzi huyo a
📌 Kaynak
Bu özet BBC Swahili kaynağından otomatik derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.
Orijinal haberi oku →