Tunachojua kuhusu mashambulizi mapya kati ya Marekani na Iran
Mashambulizi haya ya hivi karibuni yanatokea wakati mazungumzo ya kusitisha mapigano yamekwama, baada ya juhudi za kumaliza miezi kadhaa ya mapigano kushindwa kuleta maendeleo yoyote mwishoni mwa wiki.
Jeshi la Marekani limesema lilifanya mashambulizi ambayo limeyataja kuwa ya "kujilinda" dhidi ya Iran, baada ya Iran kurusha makombora ya balistiki na ndege zisizo na rubani zilizolenga meli na nchi za Ghuba.
Mashambulizi hayo yalifanyika kwenye Kisiwa cha Qeshm, kilichopo katika Mlango wa Bahari wa Hormuz. Kwa mujibu wa Kamandi Kuu ya Marekani (CENTCOM), yalikuwa "jibu kwa majaribio ya Iran ya kuanzisha mashambulizi kote Mashariki ya Kati."
Kwa upande wake, Iran ilisema ilirusha makombora na droni dhidi ya vituo vya kijeshi vya Marekani na helikopta zake katika "nchi moja ya eneo hilo," ikidai kuwa ilikuwa ni hatua ya kulipiza kisasi.
CENTCOM ilisema Tehran ilirusha makombora mawili kuelekea Kuwait na mengine matatu kuelekea Bahrain, lakini yote yaliharibika angani au yalidunguliwa kabla ya kufikia malengo yake.
Mashambulizi haya ya hivi karibuni yanatokea wakati mazungumzo ya kusitisha mapigano yamekwama, baada ya juhudi za kumaliza miezi kadhaa ya mapigano kushindwa kuleta maendeleo yoyote mwishoni mwa wiki.
CENTCOM pia ilisema kuwa shambulio la Kisiwa cha Qeshm lililenga kituo cha ardhini kinachotumiwa na vikosi vya Iran kuongoza na kuratibu operesheni za kijeshi. Aidha, jeshi la Marekani lilisema lilidungua ndege tatu za kivita za Iran ambazo zilikuwa zikilenga meli za kiraia zilizokuwa zikisafiri kihalali katika maji ya eneo hilo.
Jeshi la Iran (IRGC) limesema kwamba, "kuvuruga usalama wa Mlango wa Bahari wa Hormuz kutazigharimu vikosi vamizi vya Marekani kwa kiasi kikubwa."
CENTCOM pia ilisema kuwa Iran ilirusha makombora kadhaa ya balistiki kuelekea nchi za eneo hilo. "Makombora mawili yaliyofyatuliwa kutoka Iran kuelekea Kuwait yalipoteza mwelekeo au yalivunjika yakiwa angani, huku makombora matatu yaliyolengwa Bahrain yakidunguliwa haraka na mifumo ya ulinzi wa anga ya Marekani na Bahrain."
Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.
Iran imekuwa ikifanya mashambulizi mara kwa mara dhidi ya malengo yaliyopo Bahrain na Kuwait, ambako kuna vituo vya kijeshi vya Marekani.
Mapema, CENTCOM ilisema ilikuwa imeishambulia na kuisimamisha meli iliyokuwa ikielekea Iran, ambayo haikuwa imebeba mzigo wowote. Hatua hiyo ilikuwa sehemu ya mzingiro wa kijeshi wa majini wa Marekani katika Mlango wa Bahari wa Hormuz, ulioanza tarehe 13 Aprili.
Kwa mujibu wa CENTCOM, ndege ya kijeshi ya Marekani ilirusha kombora la aina ya Hellfire katika chumba cha injini cha meli hiyo yenye bendera ya Botswana, baada ya wafanyakazi wake "kupuuza maonyo ya mara kwa mara."
CENTCOM pia ilitoa video ambayo ilisema inaonesha wakati meli
📌 Kaynak
Bu özet BBC Swahili kaynağından otomatik derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.
Orijinal haberi oku →