Aina mpya ya ugonjwa wa kisukari unaowapasua vichwa wataalamu
Madaktari walimwambia Noella alikuwa na kisukari aina ya 5, ambayo huwaathiri vijana hususan wale walio na uzani mdogo sana.
Madaktari walipomchoma Noella Mukumbi sindano ya insulin mara ya kwanza, walidhani wananusuru maisha yake. lakini mwanamke aliye na umri wa miaka 30- kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo anasema tiba hiyo ilimfanya ajihisi kana kwamba anafariki dunia.
Noella, msusi na mama wa wattoeo wawili, alipatikana na kisukari aina ya type 1 mwaka 2023, lakini kuna kitu ambacho hakikuwa sawa.
Anasema alipoanza kutumia sindano ya insulin ya kila siku, alipatwa na kisunzi na kukosa uwezo kudhibiri mwili wake. Siku moja alizimia.
"Nilikuwa nawafulia nguo wanangu lakini nume wangu alinipata sakafuni kipiga mayowe," aliiambia BBC.
Maiaka mitatu baadaye wataalamu walimwambia huenda ana kisukari aina ya type 5.
Ugonjwa wa kisukari, unaoathiri zaidi ya watu milioni 830 kote duniani, humpata mtu wakati mwili unaposhindwa kudhibiti ipasavyo sukari ya damu kupitia insulini, kumaanisha kwamba viwango vinaweza kuwa juu na hatarisha hali ya afya.
Kisukari ya type 5 ni aina ya ugonjwa unaoaminika kutokana na lishe duni kwa muda mrefu, haswa utotoni na ujanani.
Shirikisho la Kimataifa la Kisukari (IDF), ambalo linajumuisha vyama 251 vya kitaifa vya kisukari, lililitambua rasmi aina hiyo ya kisukari mwaka jana.
Hata hivyo, Shirika la Afya Duniani (WHO) halitambui hali hii, kwa sababu bado hakuna ushahidi wa kutosha kuthibitisha kwamba ni aina tofauti ya ugonjwa huo.
Wanasayansi wengine wanaamini kuwa kisukari aina ya type 5 inaweza kuathiri hadi wagonjwa milioni 25, na wanaonya kuwa kuichanganya na aina nyingine ni hatari.
Dk. Meredith Hawkins, mkurugenzi wa Taasisi ya Kisukari Duniani katika Chuo cha Tiba cha Albert Einstein, anaamini kwamba uainishaji mbaya ni "tatizo lililoenea sana" ambalo husababisha vifo kutokana na tiba duni ya insulini.
"Baadhi ya wagonjwa tuliotangamana nao mara kwa mara hawakuamka tena siku iliyofuata," anasema.
Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.
Kisukari kinatokea wakati kongosho haizalishwi au haifanyi kazi ipasavyo, hivyo kusababisha sukari kujilimbikiza katika damu.
Katika aina ya kwanza (Type 1) kisukari kinatokea wakati kongosho haizalishwi au haifanyi kazi ipasavyo, hivyo kusababisha sukari kujilimbikiza katika damu.
Na katika aina ya 2 (Type 2), kinatokea kongosho inapokuwa haitoi insulini ya kutosha au homoni haifanyi kazi vizuri.
Hata hivyo, wanasayansi wanasema kwamba aina ya 5 ya kisukari inaweza kuhusishwa na utapiamlo wa muda mrefu, unaoathiri ukuaji wa kongosho, chombo kinachozalisha insulini.
Wagonjwa hawa bado wanaweza kutoa insulini, lakini haikidhi mahitaji ya mwili.
Kutokana
📌 Kaynak
Bu özet BBC Swahili kaynağından otomatik derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.
Orijinal haberi oku →