Kushuka kwa takwimu rasmi za Ebola ni habari njema, lakini hatari bado ipo
Kupungua huko kunatokana na data bora zaidi, baada ya maabara kuweza kuwatenga wagonjwa wengi waliokuwa na homa lakini wakisumbuliwa na magonjwa mengine kama malaria, ambayo ni ya kawaida DRC.
Takwimu za hivi karibuni za Ebola kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo zinaonekana kutoa matumaini baada ya idadi ya visa kupungua kwa kiasi kikubwa.
Awali, mamlaka zilikuwa zikizungumzia zaidi ya visa vinavyoshukiwa 1,000 na karibu vifo vinavyoshukiwa kuwa 250.
Sasa zinaripoti takribani visa 380 vilivyothibitishwa nchini DRC, ikiwemo vifo 60, pamoja na visa vingine 15 vilivyothibitishwa na kifo kimoja nchini Uganda.
Hata hivyo, tofauti muhimu ni kwamba sasa mamlaka zinazungumzia visa vilivyothibitishwa, badala ya vinavyoshukiwa kama ilivyokuwa awali.
Kwa hiyo ni kosa kudhani kushuka kwa idadi kunamaanisha mlipuko huo umepungua hatari ghafla.
Kupungua huko kunatokana na data bora zaidi, baada ya maabara kuweza kuwatenga wagonjwa wengi waliokuwa na homa lakini wakisumbuliwa na magonjwa mengine kama malaria, ambayo ni ya kawaida DRC.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus, amesema mlipuko huo ulikuwa na “mwanzo wa haraka sana” lakini timu za kushughulikia sasa “zinaanza kuufikia”.
Hata hivyo, mojawapo ya changamoto kubwa bado ni ufuatiliaji wa watu waliokaribiana na wagonjwa.
Ni takriban asilimia 45 tu ya watu waliokaribiana moja kwa moja na mgonjwa wa Ebola wanafuatiliwa kwa sasa, kwa sehemu kutokana na eneo la chanzo cha mlipuko kuwa katika eneo lililoathiriwa na migogoro.
'Ebola imetutesa': Hofu yatanda mashariki mwa DR Congo huku virusi hatari vikienea
📌 Kaynak
Bu özet BBC Swahili kaynağından otomatik derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.
Orijinal haberi oku →