Urafiki au kujiimarisha: Kwanini Xi Jinping anazuru Korea Kaskazini?

📌 Diğer 📰 BBC Swahili 🕐 3 saat önce
Urafiki au kujiimarisha: Kwanini Xi Jinping anazuru Korea Kaskazini?

Beijing inajaribu kurejesha ushawishi wake dhidi ya mshirika muhimu wa kimkakati asiyetabirika.

Kwa kiongozi wa China Xi Jinping, Korea Kaskazini ni jirani ambaye China haiwezi kumdhibiti wala kudhubutu kumpoteza.

Pande hizo mbili mara nyingi huelezea uhusiano wao kama "uliotokana umwagikaji wa damu", kumbukumbu ya Vita vya Korea.

Lakini katika miaka ya hivi karibuni, kutoaminiana kumezorotesha uhusiano huo. Na sasa Beijing inajaribu tena kuhuisha uhusiano na mshirika huyu muhimu wa kimkakati lakini asiyetabirika.

China inataka utulivu kwenye mpaka wake na ushawishi huko Pyongyang, lakini bila kuingizwa katika migogoro iliyochochewa na malengo ya nyuklia ya Korea Kaskazini.

Kwa hivyo ziara ya Xi wiki hii huenda isiwe ya kiurafiki vela bali kuhusu kujiimarisha.

Seoul anaamini kuwa anaweza kumtumia China kama mpatanishi kati ya Korea Kaskazini na Marekani, lakini Beijing huenda ina nia nyingine.

Duru za kidiplomasia za nchi za Magharibi zinaiambia BBC kwamba China imezidi kuwa na wasiwasi kuhusu kuongezeka kwa ushirikiano kati ya Pyongyang na Moscow.

Baada ya kukutana na Rais wa Urusi Vladimir Putin wiki iliyopita, huenda Xi akataka kuhakikisha pia anamdhibiti kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un, hasa wakati Beijing ikiongeza uwepo wake katika jukwaa la kimataifa.

Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.

Mvutano kati ya Beijing na Pyongyang ulionekana, hata kama ulikuwa wa hila.

Hawakuadhimisha miaka 75 ya uhusiano wa kidiplomasia mnamo Oktoba 2024.

Balozi wa China hakuhudhuria sherehe za kuanzishwa kwa Korea Kaskazini mwezi uliopita. Hakukuwa na mawasiliano ya ngazi ya juu kwa kipindi cha mwaka mzima, tofauti kabisa na uhusiano wa usuhuba kati ya Pyongyang na Moscow.

Ukaribu huo na Urusi unaoendelea kushamiri unaonekana kuikosesha Beijing usingizi.

Baada ya uvamizi wa Urusi nchini Ukraine, Korea Kaskazini imepanua ushirikiano wa kijeshi na Putin, na kilele chake imekuwa makubaliano ya ulinzi wa pande zote ambayo yalitiwa saini wakati wa ziara ya Putin huko Pyongyang mnamo 2024.

Takriban wanajeshi 2,300 wa Korea Kaskazini wamefariki wakipigania Urusi nchini Ukraine, kulingana na uchunguzi wa BBC. Pyongyang pia inashutumiwa kwa kutoa silaha kusaidia juhudi za vita za Urusi badala ya mafuta na misaada, jambo ambalo limeitia wasiwasi Washington na washirika wake, na kuishinikiza China kimya kimya.

"China inataka kuhakikisha kwamba maslahi yake dhidi ya Korea Kaskazini yanalindwa katika ushirikiano kati ya Moscow na Pyongyang," anaongeza Ankit Panda, mtaalamu wa sera za nyuklia katika Shirika la Carnegie kwa Amani ya Kimataifa.

Kwa hivyo Beijing haingelitaka kutoa na fasi kwa Urusi kuimarisha ushawi

📌 Kaynak

Bu özet BBC Swahili kaynağından otomatik derlenmiştir. Tamamı için orijinal habere gidin.

Orijinal haberi oku →
📱
News AI World — Mobil uygulama
Bu haberleri 45 dilde, anlık çeviriyle cebinde. Erken erişim için Gmail adresini bırak.
← Tüm haberlere dön